Rais Samia afanya mabadiliko Baraza la Mawaziri
- Amefanya mabadiliko madogo yaliyohusisha wizara tatu.
Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyohusisha wizara tatu kwa mawaziri wake kubadilishiwa majukumu.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus katika taarifa yake iliyotolewa Machi 31, 2022 amesema katika mabadiliko hayo aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, George Simbachawene amehamishiwa Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera na Uratibu.
Nafasi ya Simbachawene imechukuliwa na Dk Damas Ndumbaro, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.
Rais Samia amemteua Balozi Dk Pindi Chana kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii akitokea Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera na Uratibu.
Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa mabadiliko hayo yaanza mara moja.
Latest
