Facebook yabuni mfumo mpya wa kupambana na matapeli mtandaoni

July 19, 2019 12:18 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Amebuniwa baada ya kushtakiwa na mwanzilishi wa Money Saving Expert, Martin Lewis.
  • Unasaidia kubaini na kudhibiti matangazo yasiyo halisi.
  • Unasaidia kuwaepusha watu na wizi mtandaoni unaofanywa na matapeli.

Wiki hii mtandao wa kijamii wa facebook umeanzisha mfumo mpya wa kubaini na kudhibiti matangazo bandia  yanayotumia na baadhi ya watu kufanya utapeli mtandaoni.

Mfumo huo mpya unakuja baada ya mtandao huo kushtakiwa  Aprili, 2018 na mwazilishii wa tovuti ya matangazo ya  Money Saving Expert, Martin Lewis kuhusu picha zake kutumiwa kwenye matangazo bandia yaliyowekwa kwenye mtandao huo wa kijamii.

Martin amesema matangazo hayo yaliharibu heshima yake kwenye jamii lakini mwanzoni mwa mwaka huu aliamua kuachana na kesi hiyo dhidi ya Facebbok kwa masharti mawili.


Zinazohusiana:Facebook kuanza kuwachaguliwa wafuasi wake viongozi wa makundi


Aliitaka Facebook ichangie Paundi milioni 3 sawa na takriban Sh8.6 bilioni kwa ajili ya kuanzisha programu ya kupambana na udanganyifu nchini Uingereza na uazishwaji wa laini ya simu (Citizen Advice Scam Action (CASA)) kwa ajili ya kuwasaidia watu wanapokutana na udanganyifu au utapeli mtandaoni.

Ili kuweza kutumia programu hiyo, utalazimika kwenda upande wa kulia wa mtandao huo wa facebook kwenye kila tangazo ambapo utakutana na alama za nukta itatu  ukiponyeza utapata  maelezo ya kuripoti tangazo bandia (Misleading or Scam) ambayo yatasaidia Facebook kupitia malalamiko yako na kuyafanyia kazi. 

Huenda mfumo huo ukawasaidia watu wengi ambao wamekuwa wakikutana na matapeli au watu wenye nia mbaya ya kujipatia fedha kwa njia isiyo halali kwa kutumia mtandao wa Facebook. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV