Mauzo soko la hisa Dar yapaa

July 22, 2019 2:27 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Yameongezeka kwa asilimia 99.9 hadi kufikia Sh948.4 milioni kutoka Sh506,500 iliyorekodiwa mwishoni mwa wiki inayoishia Julai 19, 2019.
  • CRDB yaongozwa kwa mauzo yanayofikia Sh467.9 milioni.

Dar es Salaam. Mauzo katika soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) yameongezeka kwa asilimia 99.9 hadi kufikia Sh948.4 milioni kutoka Sh506,500 iliyorekodiwa mwishoni mwa wiki inayoishia Julai 19 mwaka huu huku benki ya CRDB PLC ikiongoza kwa kuuza hisa nyingi. 

Ripoti ya siku ya DSE iliyotolewa leo (Julai 22, 2019) inaonyesha kuwa kupanda kwa mauzo hayo kumetokana na ongezeko la idadi ya hisa zilizouzwa leo sokoni. 

Idadi ya hisa zilizouzwa leo sokoni zilikuwa 4,596,080 ambapo zimeongezeka kutoka hisa 281 zilizouzwa Julai 19 wakati soko linafungwa. 

Katika mauzo hayo ya leo, benki ya CRDB ndiyo imekuwa kinara wa kuuza hisa nyingi ikiwa ni asilimia 98.4 ya hisa zote na kuifanya iongoze kwa mauzo kwa kuweka kibindoni Sh467.9 milioni ya mauzo yote. 

Kampuni nyingine ambazo zilikuwa na mauzo ya juu ni pamoja na kampuni ya bia Tanzania (TBL) iliyouza hisa zenye thamani ya Sh283.2 milioni, kampuni ya sigara ya TCC (Sh134.8 milioni) na TPCC (Sh58.6 milioni). 

Kutokana na mauzo hayo ya leo, mtaji wa soko hilo umeongezeka hadi kufikia Sh19.2 trilioni kutoka Sh18.9 trilioni yaliyorekodiwa ijumaa iliyopita.


Zinazohusiana: 


Wakati mauzo ya DSE yakiongezeka, kampuni ya Acacia imefanya vizuri sokoni leo baada ya thamani ya hisa zake kuongezeka na kuwafanya wawekezaji wa kampuni hiyo kulala na tabasamu kwa kupata Sh350 kwa kila hisa moja. 

Hisa moja ya Acacia imeuzwa kwa Sh6,350 kutoka Sh6,000 iliyorekodiwa ijumaa iliyopita lakini kampuni hiyo haikufanikiwa kuuza hata hisa moja leo sokoni. 

Kampuni nyingine ambazo thamani ya hisa zake imepanda ni pamoja na Kenya Airways ambayo imepanda kwa asilimia 4.76, TPCC (asiulimia 3), benki ya KCB (asilimia 2.33) na kampuni ya bia ya Afrika Mashariki-EABL (asilimia 0.23). 

Hata hivyo, wawekezaji wa kampuni ya USL watalala na maumivu baada ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kushuka kwa asilimia 50 akifuatiwa na kampuni ya JHL ambayo hisa zake zimeshuka kwa asilimia 0.61.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
31 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
31 May, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

Nukta TV

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

Nukta TV

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

Nukta TV