Magufuli aagiza mradi wa umeme wa Rufiji kukingwa na bima ya Serikali

July 26, 2019 9:47 am · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Aziambia taasisi zinazohusika na mradi huo “ole wenu bima hiyo asaini mtu mwingine”.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameagiza mamlaka zinazohusika na usimamizi wa mradi wa ufuaji umeme kwa maporomoko ya maji wa Rufiji kuhakikisha kuwa unakingwa na bima ya Serikali.

Rais aliyekuwa anahutubia katika uwekaji wa jiwe la msingi la mradi huo leo (Julai 26, 2019) amesema kumekuwa na mabishano baina ya Shirika la Bima la Taifa (NIC), Tanesco, wizara na wakandarasi kuhusu huduma za bima.

Hata hivyo, Rais hakueleza kwa kina mvutano huo wa bima baina ya taasisi hizo.

“Bima ya mradi huu asilimia 100 lazima itolewe na Serikali. Kwa hiyo Waziri (Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani) hili ulizingatie, wizara ya fedha mlizingatie, Tanesco mlizingatie…ole wenu mkatafute, akasaini bima na mtu mwingine,” amesema Rais Magufuli na kuongeza;

“Huu ni mradi wa Serikali na bima na guarantee (dhamana) lazima vitolewe na Serikali.”


Soma zaidi: 


Kwa mujibu wa Dk Kalemani hadi sasa Serikali imeshatoa asilimia 15 ya fedha zote za mradi huo sawa na Sh1.007 trilioni ya Sh6.5 trilioni.

Dk Kalemani amesema utekelezaji wa mradi huo unaendelea vema na iwapo kasi hiyo itaenda hivyo hivyo siku zijazo hapana shaka utakamilika ndani ya muda miezi 42 iliyopangwa ifikapo Juni 13, 2022.

Mradi huo wa kuzalisha umeme wa Megawati 2,115, unajengwa na kampuni za Misri ambazo ni El Sewedy and Arab Contractors ambazo zilishaanza hatua za awali za ujenzi miezi sita iliyopita.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV