Facebook yaingia 10 bora ya programu zinazopakuliwa zaidi mtandaoni

December 27, 2019 6:28 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Programu nyingine zilizoingia kwenye orodha hiyo ni pamoja na Messenger, Instagram, Whatsapp,Twitter, Snapchat, Tiktok na Skype.
  • Programu hizo za simu zimekuwa kiungo muhimu cha mawasiliano duniani.

Dar es Salaam. Ndoto ya kufikia malengo katika biashara ni matamanio ya kampuni yoyote duniani hasa pale yanapotimia katika muda muafaka. 

Huenda mtandao wa Facebook ukahitimisha mwaka 2019 kwa kishindo, baada ya sehemu kubwa kukamilisha mipango yake iliyojiwekea miaka 10 iliyopita. 

Mtandao huo ulioanzishwa na raia wa Marekani, Mark Zuckerberg umefanikiwa kumiliki programu tumishi za simu nne kati ya mwaka 2010 na 2019 ambazo zimekuwa kiungo muhimu cha mawasiliano duniani. 

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na kampuni ya uchambuzi wa programu tumishi ya  App Annie imeonyesha namna kampuni hiyo ilivyoweza kufikia moja kati ya malengo yake kwa kipindi cha miaka kumi, kwa kuwakutanisha watu dunia nzima kupitia mitandao ya kijamii.

Programu hizo ni Facebook ambayo imezaa Messanger, WhatsApp na Instagram zinazotumika kuunganisha ndugu, jamaa na marafiki katika maeneo mbalimbali duniani.

Pia, zimetangazwa kama programu tumishi nne zinazoongoza kati ya 10 kwa kupakuliwa na watumiaji wengi katika kipindi cha miaka 10 mfululizo.


Zinazohusiana:


Mafanikio hayo ni hatua kubwa kwa mtandao wa Facebook kwani kumekuwa na changamoto nyingi na maboresho ya mtandao huo yaliyosaidia mtandao huo kufika ile hatua iliyokusudiwa. 

Programu tumishi nyingine ambazo zimeingia 10 bora ya kupakuliwa zaidi duniani ni pamoja na Snapchat inayomilikiwa na kampuni ya Snap ya Marekani, Skype iliyopo chini ya Microsoft na Tiktok chini ya ByteDance. 

Nyingine ni Uc Browser inayomilikiwa na kampuni ya Alibaba, YouTube chini ya Google na Twitter.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV