Necta yatangaza matokeo kidato cha pili, nne 2019

January 9, 2020 2:02 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Imetangaza matokeo ya upimaji kitaifa darasa la nne,  kidato cha pili na nne ya mitihani iliyofanyika  Novemba 2019.
  • Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2019 yanaonyesha kuwa ufaulu umeongezeka kidogo kwa asilimia 1.4 kutoka ule wa mwaka 2018.

Dar es Salaam. Katibu Mkuu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde, ametangaza matokeo ya upimaji kitaifa darasa la nne,  kidato cha pili na nne ya mitihani iliyofanyika  Novemba 2019. 

Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2019 yanaonyesha kuwa ufaulu umeongezeka kidogo kwa asilimia 1.4 kutoka ule wa mwaka 2018. Licha ya ufaulu huo kuongezeka, bado takriban nusu ama asilimia 48.6 ya watahiniwa wote wa mwaka 2019 wamepata daraja la nne.

Necta imeeleza leo kuwa katika mtihani huo wanafunzi 340,914 wamefaulu mtihani kati ya wanafunzi 422,722 waliofanya mtihani huo Oktoba mwaka jana ikiwa ni sawa na asilimia 80.65 ya watahiniwa wote. 

Hii ni sawa na kusema kuwa wanafunzi 81 kati ya 100 waliofanya mtihani huo wamefaulu. 

Ufaulu huo, kwa mujibu wa Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde, ni sawa ongezeko la asilimia 1.38 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2018. Mwaka juzi asilimia 79.27 ya watahiniwa wa shule walifaulu mtihani huo.


Soma zaidi:


Takwimu za matokeo ya upimaji kidato cha pili zinaonyesha kuwa jumla ya wanafunzi 514,251 sawa na asilimia 90.04 kati ya 571,137 wenye matokeo ya upimaji wamepata ujuzi na maarifa kuwawezesha kuendelea na kidato cha tatu. Kati yao, wasichana ni  270,750 na wavulana ni 243,501.

Dk Msonde aliyekuwa akitangaza matokeo hayo leo (Januari 9, 2020) amesema pia matokeo ya upimaji kitaifa darasa la nne (SFNA) nayo yametoka.

Matokeo hayo yanapatikana katika tovuti ya Necta. Ili kuyapata matokeo ya kidato cha nne mwaka 2019 bonyeza hapa. Na ya kidato cha pili bonyeza hapa.


TANGAZO:

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV