Muujiza uliotokea chumba namba saba gerezani

April 25, 2020 9:19 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link

Filamu ya “Miracle in Cell No.7” itakufunza mambo mengi kuhusu maisha ya familia. Picha|Mtandao.


  • Ni filamu inayomhusu binti mdogo ambaye baba yake ana ulemavu wa akili.
  • Kilele cha filamu hii ni hukumu ya kunyongwa inapotolewa kwa baba huyo kwa kusingiziwa kuua mtoto wa kamanda.
  • Matumaini yanapotoweka, ndipo miujiza inapoanza. Muujiza gani utatokea kwenye chumba namba saba kwenye filamu hii?

Dar es Salaam. “Kichaa, kichaa, kichaa!” ni sauti za watoto wanaomuimbia mwanaume ambaye anacheza nao. 

Kinachoweza kukuvuta zaidi ni kuwa mwanaume huyo ambaye anaimbiwa wimbo huo wa dhihaka na watoto ni baba wa mtoto mmoja wapo. 

“Bibi, baba yangu ni kichaa?” ni swali la mtoto Nisa Aksongur kwa bibi yake Celile Toyon ambaye anamjibu kuwa “Usiseme hivyo binti.” 

“Lakini baba yangu hayupo kama baba wengine,” ni sauti inayomuonyesha mtoto huyo jinsi alivyo kwenye sintofahamu ya uwezo wa kufikiri wa baba yake.

Sintofahamu ya binti huyo inatokana na baba yake Aras Bulut ambaye hayupo vizuri kiakili. Bila shaka watoto wenzie humtania hasa pale baba yao anapokuwa anacheza nao licha ya kumdhihaki kwa nyimbo.


Zinazohusiana


Sintofahamu ya binti huyo na bibi yake inakolea baada ya baba yake kusingiziwa kumzamisha kwenye maji mtoto wa kamanda Mesut Akusta na kuhukumiwa kunyongwa. 

Visa vyote hivyo utavipata kwenye filamu ya “Miracle in Cell No.7”. Una kila sababu ya kuitazama filamu hii yenye kuvuta hisia kama miujiza itamtokea baba huyo aliyeshindwa kujitetea mahakamani kutokana na ulemavu wa akili. Unahitaji kuandaa kitambaa na tishu kwani hakika machozi yanaweza kukutoka kidogo.

“Miracle in Cell No.7” imeongozwa na Mehmet Oztekin utaikuta katika jukwaa la mtandaoni la  Netflix na inashauriwa kutazamwa na watu wenye miaka 13 na kuendelea. 

Ukikamilisha kutazama filamu hiyo, unaweza kugeukia filamu ya “Extraction” ambayo ipo tayari na inangoja utazamaji wako tayari kukutengenezea tabasamu kwenye wikiendi yako.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV