Bushungwa awaonya wanaopandisha bei ya barakoa

April 27, 2020 1:32 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya baadhi ya taasisi zisizo za kiserikali kuuza barakoa kwa bei ya juu. 
  • Amesema bei elekezi ya barakoa haitakiwi kuzidi Sh1,500.
  • Watakaokaidi kuchukuliwa hatua za kisheria.

Dar es Salaam. Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa amezionya taasisi zisizo za kiserikali (NGO) zilizopewa kibali cha kutengeneza barakoa kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa wa virusi vya Corona kuacha kuuza barakoa kwa bei ya juu ili kujinufaisha.

Bashungwa katika taarifa yake iliyotolewa leo (Aprili27, 2020) amesema baadhi ya taasisi hizo zimekuwa zikiuza barakoa hizo kwa bei ya Sh2,500 na Sh3,000 ambayo baadhi ya Watanzania hawawezi kuimudu. 

“Wamekuwa wakitoa masharti kupitia mitandao ya kijamii kuwa hawauzi barakoa chini ya bei hiyo,” amesema Bashungwa. 

Waziri huyo ameweka wazi kuwa atachukua hatua kwa taasisi hizo ambazo hakuzitaja kwa majina pale zitakapoendelea kuuza kwa bei zinazojipangia.

Waziri huyo ametoa onyo akiwa mkoani Arusha alipotembelea Viwanda vya kuzalisha nguo vya Sunflug na A to Z kuangalia hali ya uzalishaji wa barakoa katika viwanda hivyo.


Zinazohusiana


Aidha, amevitaka Viwanda hivyo kuendelea kuzalisha kwa wingi ili wananchi walio wengi wa vijijini waweze kupata vifaa hivyo vya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa korona.

Kiwanda cha Sunflug kina uwezo wa kuzalisha barakoa 25,000 kwa siku huku cha A-Z kina uwezo wa kuzalisha barakoa 15,000 kwa siku.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV