Bidhaa za mazao zachangia kupaisha mauzo nje ya nchi Tanzania

May 19, 2020 11:06 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mapato yatokanayo na mauzo nje ya nchi yaliongezeka hadi Sh23.1 trilioni machi 2020 ikilinganishwa na Sh20.3 trilioni Machi 2019.
  • Kuimarika hali ya hewa, bei ya dunia kumesaidia bidhaa za mazao kuuzwa kwa wingi.
  • Corona yashusha mauzo ya jumla ya Machi 2020.

Dar es Salaam. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema thamani ya mauzo ya bidhaa nje ya nchi katika mwaka ulioishia Machi 2020 imeongezeka kwa asilimia 12.1 yakichagizwa zaidi na bidhaa za mazao ikiwemo korosho na mkonge. 

Mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi hujumuisha bidhaa za mazao na zile zisizo za mazao ikiwemo madini ya dhahabu na almasi. 

Ripoti ya tathmini ya uchumi ya mwezi Machi 2020 iliyotolewa na benki hiyo imesema kwa ujumla mapato yatokanayo na mauzo nje ya nchi yaliongezeka hadi Dola za Marekani 9.95 bilioni (Sh23.1 trilioni) kwa kipindi hicho ikilinganishwa na dola  8.74 bilioni (Sh20.3 trilioni) iliyorekodiwa Machi 2019.

Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 12.1 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja lililochochewa na kupaa kwa thamani ya mauzo ya bidhaa za mazao.

“Thamani ya bidhaa za mazao iliongezeka hadi Dola za Marekani 1.01 bilioni (Sh2.4 trilioni) kwa mwaka ulioishia Machi ikilinganishwa na dola 569.2 milioni (Sh1.3 trilioni) katika kipindi kama hicho mwaka 2019,” imesema BoT.

Mauzo ya bidhaa zote za mazao yaliongezeka katika kipindi hicho isipokuwa kahawa,chai na tumbaku. 

BoT imeeleza kuwa kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa za mazao kumechagizwa na hali ya hewa nzuri, ongezeko la uzalishaji na matokeo ya bei nzuri katika soko la dunia. 

Aidha, thamani ya mauzo ya jumla ya bidhaa na huduma nje ya nchi pia yamechangiwa na bidhaa zisizo za mazao ikiwemo dhahabu.

Katika kipindi hicho, mauzo ya dhahabu ambayo yalikuwa zaidi ya nusu au asilimia 55.7 ya bidhaa zisizo za mazao (non-traditional goods) yaliongezeka kwa asilimia 37.9  hadi kufikia dola 2.34 bilioni (Sh5.4 trilioni).

Hata hivyo, mauzo ya bidhaa za viwandani, samaki na bidhaa za samaki yalishuka. 

Corona yavuruga mauzo ya Machi

Wakati mauzo ya bidhaa na huduma katika kipindi cha mwaka mmoja yakiongezeka, mauzo hayo kwa mwezi Machi yamepungua ikilinganishwa na mwezi uliotanguliwa wa Februari 2020.

Mauzo ya jumla yamepungua kutoka dola za Marekani 802.3 milioni (Sh1.8 trilioni) Februari 2020 hadi dola 667.6 milioni (Sh1.5 trilioni) kutokana na kupungua kwa huduma za malipo hasa katika sekta ya utalii. 

Ripoti hiyo imesema ugonjwa wa virusi vya Corona umeathiri biashara ya utalii kwa sababu shughuli za utalii zilisimama kwa muda kutokana na vikwazo vya vya watu kusafiri ili kujikinga na ugonjwa huo. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV