Corona yachangia wanafunzi 4,000 kupata mimba Kenya

June 29, 2020 12:16 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni wasichana wa shule za msingi na sekondari kutoka kaunti ya Machakos. 
  • Wamepata mimba hizo kati ya Januari hadi Mei hasa wakiwa nyumbani baada ya mlipuko wa virusi vya Corona. 

Dar es Salaam. Kumekuwa na ujumbe unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii hasa WhatsApp unaoeleza  Kenya imetangaza kuwa wanafunzi wa kike 4,000 wamepata mimba wakati wa janga la virusi vya Corona.

Ni kweli matukio hato yametokea Kenya katika vipindi tofauti, jambo linalokatisha ndoto za masomo za wasichana hao ambao wameripotiwa katika kaunti ya Machakos.

Habari hiyo iliyoandikwa kwa lugha ya Kiswahili  kwenye picha hiyo  yenye  bendera ya Kenya inaeleza kuwa “Kenya -Yatangaza mimba elfu nne (4000) za wanafunzi katika kipindi cha corona”

Huku chini ya picha hiyo kukiwa na swali linalo uliza Je kati ya mzazi na mwalimu ni nani mlezi bora?

Ukweli ni upi

Nukta Fakti imebaini ni kweli nchini Kenya wanafunzi 4,000 wamepata ujauzito katika kipindi hicho cha corona katika kaunti ya Machakos.

Afisa Watoto katika kaunti ya Machakos, Salome Muthama akihojiwa na televisheni ya Citizen amesema wanafunzi hao wa shule za msingi na sekondari  wamepata mimba kati ya Januari na Mei mwaka huu.

Pia Muthama alinukuliwa katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Azam cha nchini Tanzania  televisheni cha Azam Tv .

“Katika kaunti ya Machakosi  wakati wa corona wasichana  4,000 wamepachikwa mimba na hiyo ni namba  kubwa sana na ukizingatia ni kuanzia Januaria hadi Mei hiyo ni miezi minne tu watoto wa chini ya umri wa miaka 19 wamepata mimba,” amesema Muthama katika mahojiano hayo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV