Ugonjwa wa figo bado tishio Tanzania

March 16, 2021 10:04 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Watanzania zaidi ya 5,000 wanakadiriwa kuwa na ugonjwa sugu wa figo.
  • Njia za kujihadhari na ugonjwa huo zimetajwa zikiwa ni pamoja na kupunguza ulaji wa nyama na mayai kwa wingi.

Dar es Salaam. Taarifa za mtu kugundulika kuwa ana ugonjwa wa figo, huwa haziwafurahishi kabisa wanafamilia kwa sababu humbatana na gharama kubwa za matibabu ambazo zinaweza kuitumbukiza familia kwenye umaskini.

Mgonjwa naye huanza safari ya maisha mapya ya kubadili mtindo wa maisha ikiwemo kuanza kula baadhi ya vyakula ili kujiweka salama.

Machi 11, 2021 ilikuwa Siku ya Figo Duniani ambapo wadau mbalimbali wa afya wamezungumzia juu ya afya ya figo na nini kinatakiwa kuzingatiwa na mtu ili kuwa na figo zenye afya.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, Watoto, kupitia ukurasa wa Instagram (@elimu_ya_Afya) ugonjwa wa figo unaweza kuzuilika kwa kunywa maji walau glasi sita hadi nane kwa siku, kupunguza kula vyakula vilivyo na chumvi nyingi pamoja na kupunguza kula nyama na mayai.

Licha ya elimu hiyo kutolewa, bado haibadilishi hali ya watu ambao tayari wamepata maradhi hayo na wanapambana kujinasua katika ugonjwa huo ambao unaitesa dunia kwa sasa. 

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Dorothy Gwajima akizungumza katika tamko maadhimisho ya Siku ya Figo Machi 11 alisema zaidi ya Watanzania 5,000 wanakadiriwa kuwa wagonjwa sugu wa figo hivyo kuwashauri Watanzania kuzingatia kanuni nzuri za afya ili kuwa salama.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
30 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
30 May, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

Nukta TV

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

Nukta TV

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

Nukta TV