Unavyoweza kukabiliana na tatizo la uchovu uliopitiliza

May 18, 2021 9:16 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kwa kukaa mbali na pombe, dawa za kulevya pamoja na tumbaku.
  • Inashauriwa kuonana na daktari kwani uchovu ukiendelea, utapata changamoto za kihisia.

Dar es Salaam. Uchovu pia ni tatizo la kiafya ambalo mbali na uwezo wa kuambatana na magonjwa mengine kama homa na maumivu ya viungo, tatizo hilo linaweza kuathiri utendaji kazi wako wa kila siku na kukurudisha nyuma kimaendeleo.

Tatizo hilo ambalo kwa lugha ya kitaalamu huitwa “fatigue” ni hali ya kuhisi uchovu wa mwili na kukosa nguvu za kufanya shughuli mbalimbali.

Uchovu huo husababishwa na mambo mbalimbali lakini tovuti ya afya ya healthline.com imesema sababu kuu ni mtindo maisha, afya ya mwili na hali ya afya ya akili ya mtu.


Soma zaidi


Kwa upande wa mtindo wa maisha, mtu anaweza kupata changamoto ya uchovu ikiwa hapati muda mzuri wa kupumzika, kuwa na uzito uliopitiliza, huzuni, matumizi ya pombe mara kwa mara, matumizi ya madawa za kulevya na kushindwa kula mlo wenye virutubisho.

Afya ya mwili inaweza kusababisha uchovu pale unapokuwa na magonjwa au maambukizi. Baadhi ya magonjwa yanayoweza kumpatia mtu uchovu ni pamoja na mafua, saratani, kisukari, magonjwa ya figo, sonona na magonjwa ya ini.

Kwa upande wa afya ya akili, uchovu unaweza kusababishwa na hali ya kuwa na wasiwasi au huzuni.

Unawezaje kukabiliana na changamoto hiyo? Tazama hii video fupi kujifunza zaidi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV