Uzushi: Watu waliopata chanjo ya Corona hawatakufa baada ya miaka miwili
- Amezushiwa kuwa amesema chanjo ina madhara na waliopata watakufa baada ya miaka miwili.
- Wametumia mahojiano yake aliyofanya na kipindi cha televisheni cha France 24.
- Montagnier amekanusha kuwa alinukuliwa vibaya.
Dar es Salaam. Baada ya mtaalamu wa afya Luc Montagnier kufanya mahojiano katika kipindi cha ‘Hold up’ kinachohusu masuala ya COVID-19 nchini Ufaransa, watu wamemnukuu vibaya na kusambaza habari za uzushi kwenye mitandao ya kijamii hasa Whatsapp.
Wamemzushia kuwa amesema watu wote waliopata chanjo ya Corona watafariki baada ya miaka miwili.
Habari hiyo iliyopo kwenye mfumo wa video katika mitandao mbalimbali ikiwemo Twitter, inamhusisha mtangazaji na Montagnier ambaye ni mshindi wa tuzo ya Nobel mwaka 2008 wakiongea kwa lugha ya kifaransa kuhusu matokeo ya chanjo za Corona zilizoanza kufanya kazi mwanzoni mwa mwaka huu.
Hata hivyo, habari hiyo haina ukweli wowote kwasababu katika mahojiano hayo Montagnier aliongelea madhara ya chanjo ya Corona, lakini hakusema watu watakaopokea chanjo hiyo watakufa baada ya miaka miwili.
Baada ya video hio kusambaa mtandaoni, Montagnier aliandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter ukisema, “Were the claims misinterpreted? Does it really mean that vaccination will cause death or its consequences would make complications?”
Ujumbe huo unamaanisha kuwa “Madai yalieleweka vibaya? Yalimaanisha chanjo zitasababisha vifo au matokeo yataleta shida?”
Were the claims misinterpreted? Does it really mean that vaccination will cause death or its consequences would make complications?#COVID19
#Corona#Vaccine#Deathwithin2years#CoronaVaccination#LucMontagnier
https://t.co/lJ6xTb92W7— Luc Montagnier (@LucMmontagnier) June 5, 2021
Pamoja na kwamba Montagnier aliongelea madhara ya chanjo ya ugonjwa wa Corona, lakini hakusema mtu anapopata chanjo hiyo atakufa baada ya miaka miwili.
Uzushi: Mshindi wa tuzo ya Nobel Montagnier hajasema watu waliopata chanjo ya Corona watakufa baada ya miaka miwili
Latest