Hapana: Uviko-19 haisambai kwa maji wala kuogelea
- Wataalamu wa afya wafafanua njia kuu ya kuambukiza ni kupitia hewa.
- Washauri watu kuendelea kuchukua tahadhari zinazotakiwa.
Wataalamu wa afya kutoka Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) wameeleza kwamba ugonjwa wa Uviko-19 hausambai kwa njia ya maji au watu kuogelea pamoja katika bwawa au chanzo chochote cha maji.
Ufafanuzi huo unatokana na kuendelea kuwepo kwa imani potofu juu ya namna homa ya Uviko-19 inavyosambaa na baadhi ya watu kuanza kuamini kuwa maji au kuogelea kunaweza kusababisha wapate homa hiyo.
Kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kuupuzia afua za kudhibiti ugonjwa huo ikiwemo kupata chanjo ya Uviko-19 nchini Tanzania licha ya ukweli kuwa ugonjwa huo umeendelea kuathiri watu wengi ulimwenguni ikiwemo kupoteza maisha yao.
Hadi jana Septemba 14, 2022, WHO inaeleza watu milioni 600 wameripotiwa kuambukizwa Uviko-19 ulimwenguni kote huku watu milioni 6.4 wakipoteza maisha.
Hata hivyo, wataalamu wa afya wameonya kwamba kwa kuwa njia kuu ya kuambukizwa ugonjwa huo ni kupitia kubadilishana hewa na mtu mwenye maambukizi basi ni vema kukaa umbali wa mita moja, kuvaa barakoa na kuepuka mikusanyiko ya watu ili kuepuka ugonjwa huo.

Latest
