Serikali kuajiri walimu zaidi ya 40,000 mwaka 2022-23

September 23, 2022 7:00 am · admin
Share
Tweet
Copy Link

Dar es salaam. Huenda uhaba wa walimu wa masomo ya Sayansi na Hesabu ukapungua nchini Tanzania na kuongeza ufaulu wa wanafunzi katika masomo hayo mara baada ya Serikali kusema iko mbioni kuajiri walimu 42,697. 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Omary Juma Kipanga aliyekuwa akizungumza bungeni jijini Dodoma Septemba 22, 2022 amewaambia Wabunge kuwa tayari kimeshaombwa kibali cha kuajiri walimu zaidi ya 42,697 na kipaumbele kitakuwa kwa walimu wa Sayansi na Hesabu.

“Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) katika mwaka huu wa fedha  imeshaomba kibali cha kuajiri walimu 42,697 kipaumbele kitakuwa walimu wa masomo ya Sayansi, Hisabati na wanaojitolea,” amesema Kipanga.

Naibu Kipanga ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Esther Matiko aliyehoji kwanini Serikali haijaweka mkakati wa kuajiri walimu wa Sayansi na Hisabati ikiwa ni asilimia 33 tu ya wahitimu wa masomo hayo walioajiriwa.

Kwa mujibu wa Kipanga kati ya mwaka 2015 hadi 2022 jumla ya wahitimu 33,492 wa kada ya ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati wamehitimu katika vyuo mbalimbali huku wahitimu 13,383 ndiyo walioajiriwa na Serikali.

Shule za Serikali nchini Tanzania zimekuwa zikikabiliwa na uhaba wa walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati jambo linalosababisha ufaulu katika masomo hayo kuwa mdogo.

Itakumbukwa katika matokeo ya mtihani wa kidato cha sita yaliyotangazwa mwezi Mei mwaka huu na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) ni wanafunzi watatu pekee kutoka shule ya Serikali walioingia katika orodha ya wanafunzi kumi bora waliofanya vizuri kwenye masomo ya Sayansi.

Huenda mpango huo wa Serikali kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ukasaidia shule zake kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV