Tamisemi yaomba Sh9.14 trilioni

April 14, 2023 8:39 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Fedha hizo ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo mwaka 2023/24. 
  • Asilimia 38.1 ya bajeti hiyo kuelekezwa katika miradi ya maendeleo. 

Dar es Salaam. Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imeliomba Bunge liidhinishe Sh9.1 trilioni kwa matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo kwa mwaka 2023/24 ikiwa ni ongezeko la Sh366 bilioni kutoka bajeti iliyoombwa ya mwaka jana. 

Waziri wa Tamisemi Angellah Kairuki aliyekuwa akisoma hotuba ya makadirio na mapato ya wizara hiyo kwa mwaka 2023/24  leo Aprili 14, 2023 amewaambia wabunge kuwa kati ya fedha hizo Sh5.6  ni kwa ajili ya shughuli za kawaida huku Sh3.48 trilioni ni kwa ajili matumizi ya maendeleo.

Sasa naomba Bunge lako Tukufu likubali kuidhinisha Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2023/24 jumla ya Sh9.144 trilioni kati ya fedha hizo Sh5.65 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida yanayojumuisha mishahara ya walimu.

“Sh3.48 trilioni kwa ajili ya shughuli za maendeleo na Sh 1.06 kwa trilioni kwa ajili ya matumizi mengineyo,” amesema Kairuki bungeni jijini Dodoma.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV