Baidu yajitosa kuanza kutengeneza simu janja

May 18, 2023 8:17 am · Davis Matambo
Share
Tweet
Copy Link
  • Itazindua simu yake mpya wiki ijayo.
  • Kampuni hiyo ya vitafuta vitu mtandaoni itaongeza ushindani katika soko la simu duniani. 

Dar es Salaam. Kampuni kubwa ya teknolojia ya China, Baidu Inc inayojulikana kwa injini yake ya utafutaji na uwezo wa akili bandia, imepanua wigo wa ushindani kwa kuanza kutengeneza simu janja. 

Kupitia kitengo chake cha Xiaodu ambacho hutengeneza spika janja zinazotumia programu tumishi ya DuerOS itazindua bidhaa yake ya kwanza ya simu janja wiki ijayo, amesema msemaji wa kampuni hiyo.

Hatua hii ni sehemu ya mkakati mpana wa Baidu wa kuunda mfumo ikolojia wa vifaa vya kielektroniki unaosaidia huduma zake za mtandao na kuongeza ushindani kwa kampuni zingine kama Apple na Samsung

Simu hiyo mpya ya kisasa itakayotolewa wiki ijayo lakini bado haijatajwa jina, itatumia teknolojia ya kisasa na imeundwa ili kutumia fursa ya uwezo wa Baidu wa akili bandia. 

Pia itaunganishwa na huduma za mtandao za Baidu, ikijumuisha utafutaji, ramani na ununuzi mtandaoni. Kuingia kwa Baidu kwenye soko la simu janja ni jambo jipya licha ya kuwa lilikuwa likitegemewa na wadau wa teknolojia.

Kampuni imekuwa ikipanua matoleo yake ya vifaa vya kielektroniki kwa kasi katika miaka michache iliyopita, na bidhaa kama vile spika janja, vifaa roboti vya usafi, na hata magari ya umeme.

Kwa kuunda mfumo shirikishi wa vifaa na programu, Baidu inatarajia kutoa hali ya utumiaji iliyofungamana ambayo inashindana na zile za Apple na Samsung. Simu janja mpya ya Baidu pia itaongeza ushindani zaidi katika soko la China. 

Ingawa Apple na Samsung zote ni maarufu duniani kote na nchini China, kampuni kubwa za ndani kama Huawei, Xiaomi, na Oppo zina uwezo mkubwa kutokana na ushindani wa bei na vipengele vilivyojanibishwa (localized).

Simu mahiri mpya ya Baidu itahitaji kutoa kitu cha kipekee ili kujulikana katika soko lenye watu wengi. Licha ya changamoto, Baidu ina matumaini kuwa itafanya vizuri katika soko la simu janja.

Zaidi ya hayo, utaalam wa Baidu katika AI unaweza kuipa nguvu ya kutengeneza vipengele vipya na uwezo unaotofautisha simu janja yake ili kuongeza faida ya kiushindani.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
25 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

Nukta TV

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV