Rais Samia afanya mabadiliko Baraza la Mawaziri

April 1, 2022 4:43 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amefanya mabadiliko madogo yaliyohusisha wizara tatu.

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyohusisha wizara tatu kwa mawaziri wake kubadilishiwa majukumu.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus katika taarifa yake iliyotolewa Machi 31, 2022 amesema katika mabadiliko hayo aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, George Simbachawene amehamishiwa Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera na Uratibu.

Nafasi ya Simbachawene imechukuliwa na Dk Damas Ndumbaro, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

Rais Samia amemteua Balozi Dk Pindi Chana kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii akitokea Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera na Uratibu.

Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa mabadiliko hayo yaanza mara moja.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
6 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
6 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Fahamu kuhusu 'BIPOLAR' | Ugonjwa hatari unaoathiri na kubadili hisia

Fahamu kuhusu 'BIPOLAR' | Ugonjwa hatari unaoathiri na kubadili hisia

Nukta TV

Je, ’BIPOLAR’ ina uhusiano na kupenda kufanya tendo la ndoa zaidi?

Je, ’BIPOLAR’ ina uhusiano na kupenda kufanya tendo la ndoa zaidi?

Nukta TV

Hii ndio sababu uhusiano wa kimapenzi ni marufuku makazini

Hii ndio sababu uhusiano wa kimapenzi ni marufuku makazini

Nukta TV