Zuhura Yunus: Mkurugenzi mpya Mawasiliano Ikulu

February 1, 2022 7:50 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Anachukua nafasi ya Jaffar Haniu ambaye atapangiwa kazi nyingine.
  • Zuhura alikuwa mtangazaji wa BBC Swahili kabla ya uteuzi huo.

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Zuhura Yunus Abdallah kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Kabla ya uteuzi huo, Zuhura alikuwa Mtayarishaji wa Vipindi na Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Rekodi aliyoiacha Zuhura ambaye alifanya kazi BBC kwa miaka 14 tangu mwaka 2008 ni kuwa mwanamke wa kwanza kutangaza kwenye kipindi cha Dira ya Dunia.

Uteuzi wake ya kuondoka BBC na kuandika kitabu chake cha wasifu wa Biubwa Amour Zahor mwanaharakati mwanamke wa kisiasa wakati wa mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964.

Zuhura anachukua nafasi ya Jaffar Haniu ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Haniu anaachia nafasi hiyo baada ya kudumu kwa takriban miezi nane tangu ateuliwe Juni 2021 akichukua nafasi ya Gerson Msigwa ambaye sasa ni Msemaji Mkuu wa Serikali.

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu amesema uteuzi huo umeanza Januari 30, 2022.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV