Zuhura Yunus: Mkurugenzi mpya Mawasiliano Ikulu

February 1, 2022 7:50 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Anachukua nafasi ya Jaffar Haniu ambaye atapangiwa kazi nyingine.
  • Zuhura alikuwa mtangazaji wa BBC Swahili kabla ya uteuzi huo.

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Zuhura Yunus Abdallah kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Kabla ya uteuzi huo, Zuhura alikuwa Mtayarishaji wa Vipindi na Mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Rekodi aliyoiacha Zuhura ambaye alifanya kazi BBC kwa miaka 14 tangu mwaka 2008 ni kuwa mwanamke wa kwanza kutangaza kwenye kipindi cha Dira ya Dunia.

Uteuzi wake ya kuondoka BBC na kuandika kitabu chake cha wasifu wa Biubwa Amour Zahor mwanaharakati mwanamke wa kisiasa wakati wa mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964.

Zuhura anachukua nafasi ya Jaffar Haniu ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Haniu anaachia nafasi hiyo baada ya kudumu kwa takriban miezi nane tangu ateuliwe Juni 2021 akichukua nafasi ya Gerson Msigwa ambaye sasa ni Msemaji Mkuu wa Serikali.

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu amesema uteuzi huo umeanza Januari 30, 2022.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW