Zigo linalomsubiri Ndejembi Ofisi ya Makamu wa Rais Tanzania

August 29, 2026 11:51 am · Method Allen
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kusimamia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050

Dar es Salaam. Hatimaye Tanzania imepata Makamu wa Rais mpya, baada ya kuapishwa kwa Deogratius Ndejembi, leo Agosti 29, 2026 ikulu ya Chamwino, Dodoma.

Ndejembi aliyekuwa Waziri wa Nishati kwa takribani miezi tisa anaziba nafasi ya Makamu wa Rais iliyokuwa wazi kwa siku mbili baada ya aliyekuwa akihudumu katika nafasi hiyo Dk Emmanuel Nchimbi kutangaza kujizulu kabla ya  kufukuzwa uanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) suala lililomuengua katika nafasi hiyo.

Akizungumza katika hafla ya uapisho wa Ndejembi Rais Samia Suluhu Hassan amesema matarajio ya watanzania ni kuona mteule huyo analitumikia Taifa kwa kutanguliza mbele maslahi ya nchi.

“Matamanio na matarajio yetu sote Watanzania kama nilivyotangulia kusema ni kwamba utalitumikia Taifa hili kwa utii, uaminifu, uzalendo, busara, hekima, maarifa na uzoefu ulio nao ukimtanguliza mbele mwenyezi Mungu na kwa maslani ya Taifa,” amesema Rais Samia.

Punde baada ya kuapishwa Ndejembi ataanza rasmi kuwatumikia Watanzania katika nafasi ya Makamu wa Rais lakini ni masuala yapi makubwa yanayomsubiri kiongozi huyo?

Kusimamia utekelezaji wa Dira ya 2050

Kama msaidizi wa kiongozi mkuu wa nchi Ndejembi atawajibika kusimamia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ambapo pamoja na mambo mengine inalenga kufikia uchumi wa Dola za Marekani trilioni moja.

Zigo kubwa linalomsubiri Ndejembi katika utekelezaji wa dira hiyo ni presha kubwa ya kiuchumi inayosababishwa na vita vya mashariki ya kati, kati ya Israeli, Marekani na Irani vinavyosababisha bei ya mafuta pamoja na bidhaa muhimu kuendelea kupaa nchini.

Licha ya changamoto  hizo mchambuzi wa uchumi kutoka Dar es Salaam Paul Chengula amesema kibarua pekee alichonacho ni kumshauri Rais namna bora ya utekelezaji wa dira hiyo pamoja na mipango  mingine ya maendeleo.

“Tutegemee makubwa kwa sababu ni nguvu mpya inaingia, yale ambayo Rais pamoja na Serikali wamekwisha kuyaanza, yeye anaweza kuyaendeleza kwa kumshauri vizuri Rais pamoja na Serikali ili kufikia malengo ya Dira ya 2050,” amesema Chengula.

Ndejembi atawajibika kusimamia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ambapo pamoja na mambo mengine inalenga kufikia uchumi wa Dola za Marekani trilioni moja | Picha Ikulu Mawasiliano

Kusimamia masuala ya muungano

Mchambuzi wa masuala ya siasa na diplomasia Efron Mkungilwa amesema  Ndejembi anajukumu la kusimamia masuala ya muungano kwa kuwa yapo ndani ya ofisi yake.

“Mambo yanayokuwa yakizungumzwa ambayo yanataka kuigawa nchi anapaswa kuiangalia na kuwaweka watu watakaoisimamia ili muungano udumu na nchi isonge mbele katika maendeleo ya nyanja zote,” ameongeza Mkungilwa.

Kusimamia utekelezaji wa katiba iliyopo

Licha ya presha ya madai ya katiba mpya iliyopo kutoka kwa wanasiasa wakongwe na wanaharakati wa upinzani, Mkungilwa amesema Serikali bado ina wajibu wa kusimamia utekelezaji wa katiba iliyopo.

kama Makamu wa Rais mpya wa Tanzania, Ndejembi anajukumu la kusimamia masuala ya muungano kwa kuwa yapo ndani ya ofisi yake na kuhakikisha watanzania wanaishi katika maono ya Serikali | Picha Ikulu Mawasiliano

Mchambuzi huyo amesiitiza kuwa wakati Serikali ikiendelea kutathimini utekelezaji wa madai hayo Ndejembi atawajibika kuisimamia katiba iliyopo ili itengeneze mifumo na watu bora.

Kwa upande wake  mchambuzi wa masuala ya kisiasa Baltazar Komba amesema umri na uzoefu wa Ndejembi vinaweza kumsaidia kuelewa lugha na matarajio ya vijana, hususani kizazi cha Gen Z na kufahamu namna rahisi ya kushughulikia changamoto zao.

“Dunia nzima leo imekuwa inapambana na hili kundi kubwa la vijana wanaojiita Gen Z, matakwa yao makubwa ni kupata riziki zinazoweza kuwafanya wajione kwamba ni sehemu ya wanaofurahia matunda ya dunia kwenye nchi zao,” amesema Komba.

Hata hivyo, Komba amesema uteuzi wa Ndejembi unapaswa kuangaliwa pia kupitia mahitaji na matarajio ya Rais aliyemteua, kwa kuwa hayo ndiyo yatakayoamua kwa kiasi kikubwa majukumu na matokeo yanayotarajiwa kutoka kwake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
20 Sep, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
20 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
20 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wakazi wa mabondeni Dar walivyojiandaa kukabiliana na ‘El Nino’

Wakazi wa mabondeni Dar walivyojiandaa kukabiliana na ‘El Nino’

Nukta TV

Wakazi Kigogo wahofia ‘El Niño’, walia mchepuo wa daraja uondolewe

Wakazi Kigogo wahofia ‘El Niño’, walia mchepuo wa daraja uondolewe

Nukta TV

Ufahamu 'BIPOLAR' Part 2 | Ugonjwa wa afya ya akili unaoweza kupelekea kifo

Ufahamu 'BIPOLAR' Part 2 | Ugonjwa wa afya ya akili unaoweza kupelekea kifo

Nukta TV