Zaidi ya Sh3 bilioni kuimarisha nishati safi ya kupikia Tanzania

February 3, 2023 1:11 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ruzuku hiyo itachochea upatikanaji wa nishati safi ya kupikia nchini Tanzania.
  • Wanufaika waaswa kuitumia ruzuku hiyo kuwafikishia wananchi nishati safi ikiwemo gesi kwa bei nafuu.

Mfuko wa Nishati Safi ya Kupikia (CookFund) Tanzania umetoa ruzuku ya Sh3.2 bilioni kwa kampuni 16 zinazotoa huduma ya uuzaji wa nishati safi ya kupikia ili kuchochea upatikanaji wa nishati hiyo Tanzania.

Ruzuku hiyo inafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) ikilenga kuimarisha teknolojia ya nishati  safi ya kupikia hususani gesi ya ‘mitungi’ yaani Liquified Petroleum Gas (LPG) na majiko ya umeme (EPC).

Pia ruzuku hiyo itaimarisha teknolojia ya  majiko ya mkaa banifu (ICS) mkaa tofali utokanao na vumbi la makaa ya mawe (briquettes) na nishati ya mafuta itokanayo na mabaki ya mimea (bioethanol).

Waziri wa Nishati, January Makamba(kushoto)akikabidhi mfano wa hundi ya ruzuku itakayoenda kuimaisha upatikaji wa nishati safi nchini.Picha|Wizara ya NishatiTwitter.

Waziri wa Nishati, January Makamba aliyekuwa akizungumza katika hafla ya kuwakadihi wanufaika hundi ya ruzuku hiyo jijini Dar es Salaam Februari 2, 2023, amewasisitiza wanufaika wa ruzuku hiyo kuzitumia fedha hizo kuleta matokeo mazuri yatakayowafikia Watanzania wengi.

“Ni vyema mkahakikisha Watanzania wananufaika kweli kupitia mpango huu kwa kuwafikishia bidhaa zenu za nishati kwa bei nafuu ili waweze kuondokana na matumizi ya nishati chafu ambazo si rafiki kwa mazingira,’’ amesema Makamba.

Hafla hiyo fupi ya fupi ya kukabidhi hundi za fedha kwa wanufaika hao ilihudhuriwa na viongozi wengine akiwemo Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Manfredo Fanti, na Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF) Tanzania Peter Malika ambaye mfuko wake ndiyo unaratibu programu ya CookFund.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
14 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV