Serikali yaanika utaratibu wa kupata mtungi wa gesi ya kupikia kwa bei ya ruzuku

February 10, 2025 5:09 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kutembelea mawakala walioanishwa na kuwa na namba ya NIDA.

Serikali ya Tanzania imesema inaendelea na zoezi la utoaji wa ruzuku ya mitungi ya gesi ya kupikia (LPG) katika maeneo mbalimbali nchini huku ikianisha utaratibu wa wa kununua gesi kwa ruzuku hiyo.

Kupitia Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia Uliozinduliwa Mei, 2024 Serikali ilibainisha kutoa ruzuku ya asilimia 20 hadi asilimia 50 ya bei ya mitungi ya gesi ili kuchochea matumizi ya nishati hiyo.

Lengo la mkakati huo ni kufikisha asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwemo gesi hadi itakapofikia mwaka 2034 kutoka asilimia chini ya 10 zilizopo sasa.

Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga aliyekuwa akijibu swali la Kabula Shitobela Mbunge wa Viti Maalum (CCM) aliyetaka kujua utaratibu unaotumika kutoa mitungi hiyo.

“Utaratibu wa sahisahivi kila mtungi mmoja unaenda kwa mtu mmoja na unachukuliwa kwa namba ya NIDA yote ni kuhakikisha tunaweza kufikisha kwa wananchi wengi zaidi,” amesema Kapinga leo Februari 10, 2025 Bungeni Dodoma.

Kapinga ameongeza kuwa utaratibu huo unatumika katika kila mkoa nchi nzima kupitia mawakala maalum walioanishwa na Serikali ambapo kufikia Februari 9, 2025 tayari mitungi 78,500 imeshatolewa kati ya mitungi 445,200 iliyotengwa huku mkoa wa Mwanza ukitengewa mitungi 19,500 kwa bei ya ruzuku.

Aidha Kapinga amebainisha mpango wa kuongeza wakala wa nishati safi ikiwemo gesi na umeme kupitia Wakala wa Umeme vijijini ili kuhakikisha wanachi wengi zaidi wanatumia nishati safi kupikia.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
12 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
12 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
12 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV