Zaidi ya nusu ya vituo vya maji havifanyi kazi Pangani

January 29, 2022 7:28 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Licha ya Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kuwa miongoni mwa maeneo yanayotegemewa kama vyanzo muhimu vya maji Tanzania, asilimia 55.1 ya vituo vya maji katika halmashauri hiyo havifanyi kazi.

Hiyo ni sawa kusema zaidi ya nusu au vituo 55 kati ya 100 katika halmashauri hiyo havifanyi kazi.

Bonde la Mto Pangani lina maeneo madogo matano ya vyanzo vya maji ambayo ni mto Pangani, Zigi, Umba, Mkulumuvi na Msangazi ambayo mito yake mikuu inamwaga maji katika Bahari ya Hindi. 

Maziwa yaliyoko katika bonde hili ni Chala, Jipe, Duluti, Manga na Karamba na Nyumba ya Mungu, Pia Mabayani na Kalimawe ni mabonde ya maji yaliyochimbwa kuhifadhi maji katika bonde hili. Bonde hili lina kilomita za mraba takriban 53,600.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW