Wazawa, wageni wanavyochuana kuitembelea hifadhi ya Ngorongoro
- Licha mchuano huo, bado watalii kutoka nje ndiyo wanaongoza kutembelea hifadhi hiyo.
- Hifadhi hiyo iko mkoani Arusha ikiwa na ukubwa kilomita za mraba 8,300.
Dar es Salaam. Watalii kutoka nje na ndani ya Tanzania wanaotembelea hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro wameendelea kuchuana huku wageni kutoka nje wakionekana kutembelea kwa wingi ukilinganisha na wazawa.
Kitabu cha Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2018 kilichotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kinaeleza kuwa jumla ya watalii kutoka nje waliotembelea Ngorongoro mwaka 2018 walikuwa 410,574 ikilinganishwa na wazawa 268,880.
Hifadhi hiyo iliyopo mkoani Arusha ikiwa na ukubwa kilomita za mraba 8,300 imekuwa kiungo muhimu kwa shughuli za utalii nchini Tanzania kutokama na vivutio vya asili kama wanyama na mimea inayopatikana ndani yake.
