Watu wanaoishi karibu na mbuga za wanyama wana afya bora: Ripoti
Kuwa na afya njema ni zaidi ya kula vizuri na kufanya mazoezi bali ni pamoja na kuishi katika eneo zuri lenye mazingira ya asili. Picha|Mtandao.
- Utafiti uliofanywa na Chuo Cha Taifa cha Oregon nchini Marekani unaeleza kuwa maeneo hayo yaliyohifadhiwa yana utajiri wa asili kwa ajili ya afya ya binadamu.
- Ni maeneo yenye utulivu na mandhari nzuri kuliko maeneo mengine.Â
- Afya bora ni zaidi ya kula chakula na kufanya mazoezi bali mazingira mazuri ya kuishi.
Yamezungumzwa mengi kuhusu umuhimu wa kula chakula bora chenye virutubisho  na kufanya mazoezi ili kuwa na afya njema na ustawi mzuri wa maisha.
Lakini ni nadra kusikia kuwa kuishi karibu na maeneo yaliyotengwa maalum na kuhifadhiwa kama mbuga za wanyama, misitu ya asili ni njia nyingine inayotumika kuboresha afya za watu.Â
Watafiti wa Chuo cha Taifa cha Oregon cha nchini Marekani, wamebaini kuwa kuishi karibu na ardhi iliyohifadhiwa ambayo inajumuisha hifadhi za Taifa, mapori ya akiba, na mbuga za wanyama kuna matokeo chanya kwa afya ya binadamu.Â
Watafiti hao wanaeleza kuwa watu wanaoishi kwenye maeneo yaliyohifadhiwa wananufaika na uhifadhi wa muda mrefu na faida hiyo huongezeka wakati eneo lilohifadhiwa linapokuwa na matumizi mengi, kwa sababu wakazi wanaweza kupata na kutumia fursa za asili za eneo husika..Â
Mtaalam wa mazingira katika Chuo hicho, Drew Gerkey  amesema mipaka ya maeneo ya uhifadhi iko katika hali inayoruhusu watu wanaoishi karibu kupata mandhari nzuri ambayo inahitajika kwa binadamu japo hawawezi kuishi ndani ya maeneo hayo.Â
Gerkey amesema maeneo yaliyohifadhiwa yenye vivutio vya utalii kama hifadhi za Taifa yana zaidi ya utajiri wa asili kwa asilimia 17 ukilinganisha na kaya ambazo ziko mbali na maeneo hayo.
Zinazohusiana:Â
- Tanzania yaangazia masoko 18 duniani kukuza utalii
- Tanzania yang’ara tena tuzo za eneo bora la utalii duniani
Matokeo ya utafiti huo ni muendelezo wa mazungumzo juu ya athari za uharibufu wa maeneo yaliyohifadhiwa ambayo ni muhimu kwa maisha ya viumbe hai.Â
Kwa mujibu wa taasisi ya Ontario Nature ya nchini Canada, maeneo yaliyohifadhiwa yana faida nyingi ikiwemo kutoa hali ya hewa nzuri, dawa za asili, burudani na utulivu ambao ni muhimu kwa maendeleo ya mwanadamu.Â
Kuwa na afya njema ni zaidi ya kula vizuri na kufanya mazoezi bali ni pamoja na kuishi katika eneo zuri lenye mazingira ya asili.Â