Watendaji wabadhirifu wizara ya ujenzi waonywa

May 3, 2021 11:53 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni wale watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
  • Waziri wa Chamuriho amesema wanachelewesha miradi ya maendeleo.

Mwanza. Serikali imesema itawachukulia hatua  watumishi watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa ubadhirifu wa fedha za miradi ya maendeleo ya umma. 

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dk Leonard Chamuriho akiwa jiji Mwanza leo Mei  3, 2021  amesema wapo watendaji  ndani  ya wizara hiyo wanashindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo na hivyo kusababisha miradi ya maendeleo kutokamilika kwa wakati. 

Dk Chamuriho amesema Serikali haitasita kuwachukulia hatua watumishi hao. 

“Nitumie nafasi hii kuwataka watumishi kufanya kazi  kwa weledi wa kazi zao na kwa kufuata misingi na maadili ya utumishi wa umma,” amesema  Waziri Chamuriho.


Zinazohusiana: 


Amesema sekta ya ujenzi  ni nguzo muhimu katika ukuaji wa uchumi na hivyo umakini wa watendaji wake unahitajika zaidi. 

“Kabla ya mwaka wa fedha 2020/2021 kukamilika Serikali itahakikisha inakamilisha miradi yote iliyokuwa imepangwa katika mwaka huu wa fedha,” amesema

Afisa Ugavi Mwandamizi sekta ujenzi, Rehema Lingo amehidi kutekeleza maelekezo ya waziri ili kuhakikisha wanasaidia katika ukuaji wa uchumi huku akiwataka watendaji kusimamia kikamilifu fedha zinazotolewa na Serikali kukamilisha miradi yote inchini. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV