Wanasayansi kuja na chanjo ya Uviko-19 ya kunywa

January 25, 2023 8:40 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Matokeo ya utafiti wa awali yaonyesha mwitikio chanya. 
  • Inatarajiwa itachochea ongezeko la watu wanaopata chanjo.

Dar es Salaam. Huenda idadi ya watu wanaopata chanjo ya Uviko-19 ikaongezeka siku za usoni pale wanasayansi watakapokamilisha utafiti wao kuhusu chanjo ya ugonjwa huo ambayo mtu anaweza kuipata kwa kunywa.

Mpaka sasa katika aina zote za chanjo zilizoidhinishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), huingizwa katika mwili wa binadamu kwa kutumia njia ya sindano jambo ambalo limekuwa kigezo kwa baadhi ya watu kutochanja kwa kuogopa maumivu ya sindano.

Kwa mujibu wa tovuti ya masuala ya teknolojia ya nchini Marekani ya Cnet watafiti na wanasayansi wameongeza nguvu katika ugunduzi wa chanjo mpya kupitia mfumo wa upumuaji au kinywa.

Chanjo hiyo itakayofahamika kama QYNDR (kinder),  imeshakamilisha sehemu ya kwanza ya majaribio yake na sasa inasubiri fedha kwa ajili ya majaribio zaidi na kisha iingizwe sokoni.

Kwa mujibu wa Kyle Flanigan ambaye ni mtengenezaji wa chanjo hiyo, ‘kinder’ itatumia njia rafiki kuingia kwenye mwili wa binadamu.

Flanigan anasema matokeo ya utafiti wa chanjo hiyo yaliyofanyika nchini New Zealand yana mwitikio chanya ingawa bado hayajakaguliwa na mamlaka za kiafya za kimataifa.

“Si rahisi kutengeneza na kuifanya  na chanjo iweze kufanya kazi kupitia mfumo wa mmeng’enyo, tuligundua njia itakayoifanya chanjo ipite tumboni na kutoa matokeo yanayofaa, “ anasema Flanigan.

Habari za uwepo wa majaribio ya chanjo za Uviko-19 kwa njia ya mfumo wa mmeng’enyo wa chakula zinakuja kipindi ambacho mzalishaji wa chanjo za Pfizer anakabiliwa na ukosoaji mkubwa nchini Marekani kuhusiana na ufanisi wa chanjo zake.

Hata hivyo mpaka sasa WHO hawajatoa taarifa yoyote ya kuthibitisha shutuma hizo dhidi ya Pfizer zaidi ya kuendelea kusisitiza matumizi ya chanjo kwani zimesaidia kuokoa mamilioni ya maisha ya watu.

Wataalamu wa afya wanaendelea kusisitiza kuwa ugonjwa wa Uviko-19 bado upo na unaua  ingawa kwa kasi ndogo ambapo kwa mujibu wa WHO Januari 23 mwaka huu watu 1,017 walipoteza maisha siku hiyo huku jumla ya watu milioni 6.7 wakipoteza maisha tangu kuanza kwa janga hilo mwaka 2019.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV