VIDEO: Usifanye haya unaposikia kiu
- Ni pamoja na kutokutumia vinywaji kama soda na juisi kwa kuwa havitosaidia kuikata kiu yako.
- Badala yake pendelea kutumia maji ya kunywa hata kama hausikii kiu.
Dar es Salaam. Mara nyingi watu wanapopata kiu hufikiria kuwa kimiminika chochote kinaweza kuikata kiu hiyo.
Wengine huharakisha kununua soda “Bariiiidi!” hasa wale wanaokuwa kwenye mizunguko yao wakifikiri kuwa kinywaji hicho kitakata kiu waliyo nayo. Kama wewe huwa unakunywa soda unaposikia kiu, unachofanya hakishauriwi kiafya.
Wataalamu wanashauri mtu kutumia maji ya kunywa pale anaposikia kiu badala ya kimiminika kingine chochote kukata kiu kwa kuwa mtu anapokuwa katika hali hiyo ni kiashiria kuwa mwili una unahitaji mkubwa wa maji na hivyo kitu pekee unachohitaji mwilini ni maji ya kunywa.
Zinazohusiana
Daktari wa mafunzo ya mazoezi tiba Dk Joshua Sultan ameiambia Nukta kuwa mtu hujisikia kiu baada ya mwili kuishiwa maji mwilini na hivyo kuhitaji maji tu badala ya kimiminika chochote kilichotiwa nakshi kama soda au juisi.
Kufahamu zaidi kuhusu kiu na namna ya kukabiliana nayo, tazama video hiii.
Latest
