VIDEO: Epuka fangasi sehemu za siri kwa kufanya haya

March 15, 2021 8:25 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kuhakikisha sehemu zako za siri zinakuwa kavu mara zote.
  • Pia inashauriwa kubadilisha nguo zako za ndani kila siku na kuepuka kuvaa nguo zilizobana.

Dar es Salaam. Hakuna kitu ambacho kinampatia mtu hali ya kutokujiamini kama kuwa na fangasi mwilini kwani kero ya muwasho, harufu mbaya, ukavu wa ngozi na michubuko, siyo jambo rahisi kuvumilika. 

Hali huwa mbaya zaidi pale fangasi hao wanapohamia baadhi za sehemu za mwili ambazo huenda kuzitibu ikawa ni changamoto kwa kuwa mara nyingi sehemu hizo hufunikwa na nguo na hivyo kupata joto kwa urahisi ikiwemo sehemu za siri. 

Kwa mujibu wa tovuti ya healthline inayoozungumzia masuala ya afya, kupata fangasi sehemu za siri ni rahisi kwa sababu fangasi huhitaji maeneno yaliyo na joto na unyevu ili kuishi.

Mara nyingi maeneo ya ndani ya mapaja, sehemu za makalio na sehemu za siri ni maeneo yanayopata fangasi kwa urahisi.

Kuepukana na hali hiyo, inahitaji mtu kukausha sehemu zake za siri mara baada ya kuoga na pia inashauriwa kama mwili wako unatoa jasho kwa wingi, paka poda ya watoto ili kuepusha unyevu sehemu hizo:

Njia zingine ni zipi? Tazama video hii

                     

Enable Notifications OK No thanks