UN Environment yaanza kutumia tovuti, mitandao ya kijamii ya Kiswahili

September 13, 2019 6:01 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Wakati Tanzania ikijipanga kukifanya Kiswahili kuwa lugha rasmi ya Afrika Mashariki, Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UN Environment) limezindua tovuti mpya na mitandao ya kijamii kwa lugha ya Kiswahili ili kuwafikia mamilioni ya wazungumzaji wa lugha hiyo kote duniani.

Mpango huo wa Tanzania ulitangazwa jana (Septemba 12, 2019) na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dak Harrison Mwakyembe ambaye amesema tayari Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) limepitisha Kiswahili kuwa lugha rasmi.

Amesema  kinachosubiriwa ni baraka za wakuu wa nchi wa jumuiya hiyo yenye nchi wanachama za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudan Kusini.

Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa nalo jana limezindua tovuti mpya na mitandao ya kijamii kwa lugha ya Kiswahili, ikiwa ni hatua ya kuikuza lugha hiyo yenye wazungumzaji zaidi ya milioni 150 duniani.

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Joyce Msuya amesema lengo ni kuwafikia mamilioni ya wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili kote duniani,  kwani tovuti hiyo ya Kiswahili na mitandao ya kijamii vitatoa taarifa za mazingira, takwimu muhimu na kuelezea hadithi zitakazowahamasisha watu wanaofanya kazi kuboresha mazingira ya dunia.

“Tovuti hiyo pia itaeleza kuhusu mada muhimu zihusuzo matatizo ya mabadiliko ya tabianchi, bayoanuai, suluhu za kiasili, uchaguzi wa hali ya hewa na mengine mengi,” inaeleza taarifa ya Msuya iliyotolewa jana.


Soma zaidi: 


Uzinduzi wa tovuti hiyo mpya ya Kiswahili na mitandao ya kijamii umefanyika siku chache kabla ya mkutano wa Umoja wa Mataifa wa kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi ambao utafanyika jijini New York, Marekani Septemba 23 mwaka huu.

Shirika la UN Environment limekuwa ni sauti inayoongoza duniani katika masuala ya mazingira. Linatoa muongozo na kuchagiza wadau kulinda mazingira, kuhabarisha na kuyawezesha mataifa na watu kuboresha hadhi ya maisha yao bila kuweka rehani mustakabali wa dunia na vizazi vijavyo kimazingira.

Katika kufanikisha azma hiyo, UN Environment inafanya kazi kwa karibu na wadau wote zikiwemo Serikali, sekta binafsi, asasi za kiraia, mashirika ya kimataifa  na mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa kote duniani.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV