Ukweli kuhusu maiti kuambukiza Corona

June 19, 2020 5:52 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Hakuna ushahidi kuwa mwili wa mgonjwa wa Corona unaweza bado kueneza maambukizi saa mbili tangu kifo kilipotokea. 
  • Unashauriwa kuwasiliana na kituo cha kutolea huduma za afya na usioshe wala kuhifadhi mwili wa mtu aliyefariki kwa Corona nyumbani.

Dar es Salaam. Ugonjwa wa wa virusi vya Corona umeibua maswali mengi kwa watu hasa jinsi ya kujikinga huku wengine wakiamua kujipa majibu ya maswali yao na pengine bila kuwa na uhakika wa wanachokisema.

Kama wewe ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii, huenda umewahi kukutana na kuziamini habari kuhusu miili ya watu waliofariki kwa COVID-19 inaweza kueneza ugonjwa huo baada ya saa mbili, basi fahamu kuwa umedanganywa.

Wazira ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika kituo chake cha mtandaoni cha taarifa za Corona imeeleza hakuna ushahidi kuwa mwili wa mgonjwa wa Corona unaweza bado kueneza maambukizi saa mbili tangu kifo kilipotokea. 


Zinazohusiana


Hata hivyo, wizara hiyo imeshauri watu kutokuhifadhi mwili wa mtu aliyefariki kwa ugonjwa wa Corona nyumbani wala kuuosha. 

Badalla yake, wawasiliane na wataalamu kwa ajili ya kupewa maelekezo muhimu.

“Usihifadhi mwili wa marehemu nyumbani, toa taarifa kituo cha kutolea huduma za afya kilichopo karibu. Pia Usiuguse wala kuosha mwili wa marehemu, Maziko yataratibiwa na wataalamu wa afya ili kuepuka maambukizi,” Imeeleza wizara hiyo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.