Ufaulu masomo manne washuka kidato cha sita

July 11, 2019 12:27 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Masomo hayo ni General Studies, Historia, Bailojia na Accountancy.
  • Ufaulu wake umeshuka kwa viwango tofauti ukilinganisha na mwaka 2018. 
  • Masomo ambayo ufaulu wake umepanda ni pamoja na Geografia, Kiswahili, English na Kemia. 

Dar es Salaam. Matokeo ya kidato cha sita mwaka 2019 yaliyotangazwa leo yanaonyesha kuwa ufaulu wa watahiniwa katika masomo manne, likiwemo la General Studies ambalo huchukuliwa poa na wanafunzi, umeshuka kwa viwango tofauti ukilinganisha na mwaka jana. 

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde ameyataja leo (11 Julai 2019) masomo ambayo ufaulu umeshuka ni pamoja na General Studies, Historia, Biolojia na Accountancy. 

Amesema ufaulu wa somo la General Studies umeshuka kutoka asilimia 94.45 mwaka 2018 hadi asilimia 92.14 mwaka huu ambapo somo la Historia, ufaulu wake umeshuka kutoka asilimia 99.05 hadi 96.91. 

Somo la Baiolojia ambalo ni miongoni mwa masomo ya sayansi ufaulu wake umeshuka kiduchu kutoka asimia 96.98 mwaka 2018 hadi asilimia 96.12 mwaka huu. 


Soma zaidi: 


Somo lingine ambalo ufaulu wake umeporomoka ni ‘Accountancy’ (Uhasibu) ambapo umeshuka kutoka asilimia 96.51 hadi asilimia 96.08 mwaka huu. 

Wakati masomo hayo manne ufaulu wake ukishuka, ufaulu wa masomo 14 yaliyobaki umepanda likiwemo somo la Advanced Mathematics ambalo limekuwa likiwatoa jasho wanafunzi wengi. 

Ufaulu wa somo hilo umepanda hadi asilimia 86.74 mwaka huu kutoka asilimia 83.74 iliyorekodiwa mwaka 2018. 

Masomo mengine ambayo ufaulu wake umepanda ni pamoja na Geografia, Kiswahili, English na Kemia. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV