UDSM yatakiwa kuongeza kasi utoaji haki miliki kwa wavumbuzi

April 26, 2019 8:31 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Sera ya umiliki wa Mali-Akili ya mwaka 2008 inataka Chuo Kikuu kupata kinga ya kisheria katika kutangaza na kuuza kibiashara bidhaa zinazohusiana na Mali-Akili kadri itakavyokuwa inafaa kwa maslahi ya Chuo, mtafiti na umma kwa jumla. Picha|Mtandao.


  • Hatua hiyo inakuja baada ya CAG kubaini kuwa kuna usimamizi na utangazaji duni wa Mali-Akili chuoni hapo.
  • Tangu mwaka 1981 hadi Januari 2018 Chuo kiliweza kutengeneza mashine 66, lakini uvumbuzi mmoja tu ndiyo ulikuwa na haki miliki.
  • Imeshauriwa kutengeneza mifumo imara ya kuchunguza vumbuzi zinazokidhi kupata haki miliki na kufikiria kutoa motisha kwa wavumbuzi bora.

Dar es Salaam. Wakati watanzania wakiungana na wenzao duniani kuadhimisha Siku ya Mali-Akili Duniani (World Intellectual Property Day), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimetakiwa kutengeneza mfumo mzuri wa usimamizi na kuendeleza vumbuzi mbalimbali zenye sifa ya kupata haki miliki. 

Siku ya Mali-Akili Duniani huadhimisha Aprili 26 ya kila mwaka ikiwa na lengo la kuchochea uvumbuzi na ubunifu katika sekta mbalimbali zinazoweza kuchangia katika maendeleo ya dunia. 

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad ya mwaka 2017/2018 kuhusu Serikali Kuu imesema kuna usimamizi na utangazaji duni wa Mali-Akili katika chuo hicho jambo linalokwamisha kasi ya ukuaji wa vumbuzi mbalimbali. 

“Tangu mwaka 1981 hadi Januari 2018, Chuo Kikuu kupitia Technology Development and Transfer Centre (TDTC) kiliweza kubuni, kutengeneza na kuhamisha mashine 66 za aina tofauti pamoja na vipengele 35,769 vya mashine. Hata hivyo, ni mvumbuzi mmoja tu alikuwa na haki miliki,’ inasomeka sehemu ya ripoti hiyo. 

Ripoti hiyo inaeleza kuwa kuanzia mwaka 2007 hadi 2018, UDSM ilitunza uvumbuzi mmoja kuhusu uchakataji wa juisi ya ndizi na utafiti huo ulihifadhiwa mnamo Septemba 16, 2009.


Soma zaidi: 


Chuo Kikuu kwa miaka mingi kiliweza kuchapisha tafiti 2,983 lakini zenye sifa ya kupata haki miliki ni chache. Hali hiyo inasababisha kushindwa kuweka wazi vumbuzi kwa ajili ya kupata haki miliki.  

“Hii ni dalili ya kuwa, Mali-Akili hazitangazwi vya kutosha na Chuo Kikuu. Hakuna namna nzuri na imara za kutathmini vumbuzi zenye matokeo yanayostahili kupewa Haki Miliki,” inaeleza ripoti hiyo.  

Sera ya umiliki wa Mali-Akili ya mwaka 2008 inataka Chuo Kikuu kupata kinga ya kisheria katika kutangaza na kuuza kibiashara bidhaa zinazohusiana na Mali-Akili kadri itakavyokuwa inafaa kwa maslahi ya Chuo, mtafiti na umma kwa jumla. 

CAG anapendekeza UDSM itengeneze mfumo madhubuti (database) ili kurahisisha ufuatiliaji na tathmini ya vumbuzi zinazofaa kupata haki miliki. 

Pia, kutengeneza mifumo imara ya kuchunguza vumbuzi zinazokidhi kupata haki miliki na kufikiria kutoa motisha kwa wavumbuzi bora katika eneo hili.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV