Trace Together: App iliyobuniwa kupambana na Corona

March 23, 2020 9:59 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Muonekano wa app wa TraceTogether inayosaidia kupata taarifa za corona. Picha|Mtandao.


  • Imezindua programu tumishi ya simu (app)  itakayowezesha Serikali kuwafuatilia na kuwatambua watu waliokaribiana na wagonjwa wa maradhi ya COVID-19 kama moja ya juhudi za kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona. 

Wakati wanasayansi duniani wakiendelea kutafuta tiba na chanjo ya ugonjwa virusi vya Corona (COVID-19), wabunifu nao wanabuni mifumo ya kidijitali itakayosaidia kuongeza ufanisi wa tahadhari za kujikinga na ugonjwa huo unaosambaa kwa kasi duniani. 

Nchi ya Singapore imezindua programu tumishi ya simu (app)  itakayowezesha Serikali kuwafuatilia na kuwatambua watu waliokaribiana na wagonjwa wa maradhi ya COVID-19 kama moja ya juhudi za kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona. 

App hiyo iliyopewa jina la TraceTogether app, ilizinduliwa jana (Machi 20, 2020) na shirika la teknolojia la serikali ya Singapore la GovTech kwa kushirikiana na wizara ya afya ambapo inaweza kupakuliwa na wananchi wa Singapore wenye namba za simu na simu janja zenye “Bluetooth”.

App hiyo itakuwa inabadilishana taarifa za watu wanaopishana barabarani kwa umbali usiozidi mita mbili kupitia bluetooth ili kutambua taarifa za mtu mwingine. 


Soma zaidi: 


Rekodi zao zitatunzwa kwenye app iliyoko kwenye simu na hazitatumwa kwa mamlaka husika. 

Watumiaji watatakiwa kutuma taarifa zao ikiwa wataombwa na Wizara ya Afya ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa kufuatilia ukaribu wa watu. Ikiwa mtu atakataa kubadilishana taarifa na wizara anaweza kushitakiwa chini ya Sheria ya Magonjwa ya Yanayoambukiza ya nchi hiyo.  

Ingawa hakuna atakayelazimishwa kuwa na app hiyo, Serikali imesema itawahamasisha watu kuwa nayo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.