TMDA yateketeza bidhaa feki zenye thamani ya zaidi ya Sh8 bilioni
Dar es Salaam. Huenda athari za kiafya zinazotokana na kutumia bidhaa zisizo na ubora ikiwemo dawa na vifaa tiba zikapungua kwa Watanzania mara baada ya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kuteketeza zaidi ya tani 14,704 za bidhaa zisizokidhi viwango vya ubora.
Kwa mujibu wa ripoti ya utendaji kazi ya TMDA ya mwaka 2021 inaonyesha tani hizo 11,704 zilizoteketezwa zilikuwa zina thamani Sh8.45 bilioni.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), nusu ya madhara yote yanayoweza kuzuilika katika huduma za afya yanahusiana na dawa.
WHO inaeleza kuwa robo ya madhara hayo yanayohatarisha maisha huku mazoea ya kutumia dawa zisizo salama na makosa ya utoaji dawa ni mojawapo ya sababu kuu za majeraha na madhara yanayoweza kuepukika katika mifumo ya huduma za afya duniani kote.
