The Devil All The Time: Filamu inayowagonganisha vichwa wapendanao

September 18, 2020 11:02 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Inamhusu kijana anayepigania kuwalinda awapendao
  • Visasi, vitimbi vya kukata na shoka na sekunde za kushikilia pumzi yako ni kati ya vitu utakavyovikuta kwenye filamu hii.
  • Kama wewe ni muoga wa filamu zenye mauaji, hii siyo kwa ajili yako.

Dar es Salaam. Kwenye kumbukizi yake ya kuzaliwa, Arvin Russell (Tom Holland) anakabidhiwa bastola na Earskell ambaye ni babu yake.

Bastola hiyo iliwahi kumilikiwa na baba yake ambaye alijiua baada ya mke wake (Mama Arvin) kufa kwa ugonjwa wa saratani na hivyo kuchukuliwa na babu yake Earskell aliyeishi na mkewe Emma pamoja na Lenora.

Mkanda unaanza kukolea baada ya Lenora kujihusisha kimapenzi na Mchungaji Preston Teagardin na kwa kuwa kitanda hakizai haramu, Lenora anapata ujauzito.

Ebo, Mchungaji Preston anaukana ujauzito huo na kumshauri autoe.


Soma zaidi


Arvin ambaye anashikwa na hasira, anamtafuta Mchungaji huyo na kumuua baada ya kufuatilia mienendo yake kwa muda mrefu na kumuona mchungaji Preston akiendelea kufukuzia mabinti wengine.

Unapitwaje na filamu hii ambayo bado inafuka moshi kwenye mtandao wa Netflix huku ikiwa imesheheni nyota wa filamu kutoka “Spider Man”, “Twighlight” na “Mad Max Furry Road”.

Hata hivyo, kama wewe siyo mpenzi wa filamu, unaweza kufuatilia burudani zingine ikiwemo albamu mpya ya Alicia Keys au nyimbo za Bongo Fleva zikiwemo za Zuchu na Diamond Platnumz zinazotikisa mtandao wa Youtube kwa sasa.

Kama hilo siyo fungu lako pia, utalii umejaa tele ukikusubiria.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV