TCRA yaifungia Jamii Forums kwa siku 90

September 6, 2025 3:31 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kutokana na kuchapisha maudhui kinyume na sheria.

Arusha. Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesitisha leseni ya kuchapisha maudhui mtandaoni ya kampuni ya Vapper Tech Limited (JamiiForums) na kuzuia upatikanaji wa jukwaa la Jamii Forums kwa siku 90.

Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dk Jabiri Bakari, iliyotolewa leo Septemba 9, 2025 inabainisha kuwa leseni hiyo imesitishwa kutokana na kuchapisha maudhui kinyume na sheria bila kubainisha maudhui yenyewe.

“Mnamo tarehe 04 Septemba 2025, Jamii Forums kupitia jukwaa lake na akaunti zake za mitandao ya kijamii ilichapisha maudhui ya kupotosha Umma, kukashifu na kudhalilisha Serikali na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinyume na Kanuni za Maudhui Mtandaoni za mwaka 2020 na Marekebisho yake ya mwaka 2022 па 2025,” imesema taarifa ya Dk Bakari.

TCRA imebainisha kuwa maudhui hayo pia yanakinzana na utamaduni, mila na desturi za Kitanzania, jambo ambalo linaathiri umoja, amani na mshikamano wa kitaifa, na kuharibu taswira ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Jamii Forums  uamuzi wa TCRA  umetokana na wao kuchapisha taarifa ya mwanasiasa Humphrey Polepole kuhusu mfanyabiashara Rostam kumiliki mgodi wa makaa ya mawe kwa asilimia 70 na taarifa za uhusiano kati ya Rais wa Tanzania na mfanyabiashara raia wa Zimbabwe Wicknell Chivayo bila kuzingatia mizania.

“Jamii Forums ilishindwa kutafuta maoni ya Mamlaka husika/Msemaji wa Rais/Serikali, kuthibitisha uhalisia wa picha (za Rais na Chivayo) zilizotumika, na hivyo kuuaminisha Umma taarifa za upande mmoja,” imesema taarifa ya Jamii Forums ikinukuu maamuzi ya TCRA.

Kwa hukumu hiyo Jamii Forums pamoja na majukwaa yake yote ya mtandaoni haitaweza kurusha taarifa za uchaguzi unaotarajia kufanyika Oktoba 29, mwaka huu kama ambavyo imekuwa ikifanya miaka.ya nyuma kwa kuwa itakuwa ndani ya kipindi cha adhabu.

Hii si mara ya kwanza kwa TCRA kufungia chombo cha habari Tanzania.

Oktoba 2024 TCRA ilisitisha  leseni zote za kuchapisha maudhui mtandaoni za kampuni ya Mwananchi Communication Ltd kwa kwa tuhuma za kuchapisha maudhui yaliyokiuka Sheria za nchi na kuleta tafsiri hasi kwa Taifa.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.