TBS mwendo mdundo utoaji huduma kidijitali

September 4, 2019 11:13 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Yazindua mfumo wa kielektroniki wa kusajili bidhaa, majengo na maeneo ya uzalishaji. 
  • Utasaidia kuokoa muda na gharama kwa waombaji na kupunguza usumbufu wa usajili uliokuwa unajitokeza hapo awali.

Dar es Salaam. Shirika la viwango Tanzania (TBS) katika kuboresha huduma zake, limekuja na mfumo mpya kielektroniki unaowaweza wananchi kupata huduma ikiwemo kufanya usajili wa bidhaa, majengo na maeneo ya uzalishaji mtandaoni.

Mfumo huo unaojulikana kama ‘TBS Online Application System (OAS)’ huenda ukawapunguzia usumbufu waombaji waliokuwa wanatumia mfumo wa kawaida na kuwawezesha kuokoa muda na gharama za usafiri kwenda kufuata huduma hiyo TBS. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TBS, mfumo huo ulianza kutumika rasmi Septemba 1, 2019 ambapo kwa sasa wateja wote wanaotaka huduma za usajili watatumia mfumo huo wakiwa popote nchini.  


Zinazohusiana:


Ili mtu aanze kutumia mfumo huo anapaswa kujisajili na kuwa na akaunti katika mfumo wa ‘OAS’ uliopo katika tovuti ya TBS na kufuata taratibu zote zilizowekwa ili kufanikisha maombi yake. 

Mabadiliko ya teknolojia, yamerahisisha maisha. Taasisi za umma na binafsi zinachukua hatua mbalimbali kutumia mifumo ya kidijitali ili kurahisisha utoaji wa huduma na bidhaa na wakati huo huo kuongeza mapato ya kampuni. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.