Tanzania kuiuzia Malawi tani 7,000 za mbaazi ghafi

June 1, 2019 11:12 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Hatua hiyo inakuja baada ya Malawi kuwa na uhitaji wa zao hilo.
  • Tayari mchakato wa oda iliyotolewa na Malawi umeanza kufanyiwa kazi. 
  • Lakini Serikali imesema inaendelea na jitihada za kujenga viwanda vya kuchakata zao hilo nchini.

Dar es salaam. Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya amesema Tanzania inakusudia kuuza tani 7,000 za mbaazi ghafi kwa nchi ya Malawi, ikiwa ni mkakati wa muda mfupi wa kutafuta masoko mbadala kimataifa. 

Mhandisi Manyanya ameeleza azma hiyo ya Serikali bungeni jana (Mei 31, 2019) wakati akijibu swali la Mbunge wa Nachingwea, Hassan Masala ambaye alitaka kufahamu mikakati ya Serikali katika kuwakwamua wakulima wa mbaazi ikizingatiwa kuwa soko la zao hilo limekuwa likisuasua. 

Akijibu swali hilo, Manyanya amesema Malawi imeonyesha dhamira ya kununua mbaazi ya Tanzania, baada ya Serikali kuzitembelea baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Malawi na Burundi ili kutafuta soko la zao hilo. 

“Mkakati wa muda mfupi ni kutafuta masoko mbadala nchi za nje ambapo mbaazi ghafi zitauzwa. Jitihada hizo zimeanza kuzaa matunda kuanzia Machi 2019, kufuatia jitihada ya Serikali ya kutafuta mazao ya kilimo ikiwemo mbaazi katika nchi za jirani za Malawi, Burundi, Congo DRC na Zambia. 


Zinahusiana:Kampuni yafungua mlango kununua chumvi ya wakulima Tanzania.


“Katika ziara hiyo nchi ya Malawi kwa mwaka huu imeonyesha uhitaji wa tani 7,000 na taratibu za kuhakikisha oda hiyo inatekelezwa zinaendelea,” amesema Mhandisi Manyanya. 

Akizungumzia mkakati wa muda mrefu, amesema wanaendelea kuhamasisha  jitihada za uwekezaji wa viwanda vya kukoboa na kuongeza thamani ya mazao ya mbaazi na mazao mengine ya jamii ya mikunde hapa nchini.

Amebainisha kuwa kampuni ya Mahashree Agro Processing Ltd kutoka nchini India inajenga kiwanda mkoani Morogoro ambapo hadi kufikia Juni mwaka huu, kiwanda hicho kinategemewa kuanza kazi huku kikiwa na uwezo wa kuchakata na kusindika tani 700,000 kwa mwaka.

Amesema viwanda vingine viwili  vimeshaanza kufanya kazi vya Power Quality Exporters Limited kilichopo Dar es salaam na kiwanda cha Samson Agro Export limited.

Muonekano wa mbaazi baada ya kumenywa. Picha | Mtandao

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV