Tahadhari: Unene uliopitiliza unaweza kumpata kila mtu

September 30, 2020 7:24 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Tatizo hilo linaweza kumpata mtu yoyote duniani.
  • Unene uliopitiliza huchangia kupata kisukari, kiharusi na magonjwa ya moyo.
  •  Shirika la Afya Duniani (WHO) lataka mshikamano kumaliza tatizo hilo.

Dar es Salaam. Kama bado una fikra kuwa unene uliopitiliza (obesity) unawapata watu wenye kipato kizuri hasa katika nchi zilizoendelea duniani, utakuwa unajidanganya. 

Kwa sasa, tatizo hilo linawapata watu wote hata wasio na fedha katika nchi maskini. 

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema tatizo hilo la kiafya limesamba kila mahali duniani ambapo takriiban watu milioni 2.8 hufariki dunia kila mwaka kutokana na unene uliopitiliza. 

“Zamani ulikuwa unahusishwa na nchi zenye kipato cha juu (high-income countries), kwa sasa unene uliopitiliza unawakumba hata watu waliopo kwenye nchi zenye kipato cha kati na chini,” inaeleza WHO.

Shirika hilo imezitaka serikali, washirika wa kimataifa, asasi za kiraia, mashirika yasiyo ya kiserikari na sekta binafsi kushikamana kuzuia na kupunguza tatizo la unene uliopitiliza. 

Unene uliopitiliza huchangia kupata magonjwa ya kisukari, moyo na kiharusi.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW