Shule za msingi, sekondari kufunguliwa Juni 29

June 16, 2020 1:33 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya kupungua kwa ugonjwa wa virusi vya Corona Tanzania. 

Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameagiza kufunguliwa kwa shule zote za awali, msingi na sekondari ifikapo Juni 29 mwaka huu zilizokuwa zimefungwa kwa miezi mitatu kutokana na janga la virusi vya Corona kwa sababu ugonjwa huo umepungua kwa kiasi kikubwa nchini Tanzania. 

Rais Magufuli aliyekuwa akizungumza leo (Juni 16, 2020) jijini Dodoma wakati akifunga Bunge la 11, amesema maisha na shughuli zingine ikiwemo masomo lazima yaendelee kama kawaida. 

“Kutokana na hali ya ugonjwa wa Corona kuendelea vizuri na kwa kweli imepungua sana. Napenda nitumie nafasi kutangaza kwamba kuanzia tarehe 29 nafikiri itakuwa Jumatatu mwezi huu wa Juni shule zote zifunguliwe zilizokuwa zimebaki,” amesema Dk Magufuli.

Serikali ilifunga shule na vyuo vyote nchini Machi mwaka huu ili kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo wa COVID-19. 

Juni mosi, Rais aliruhusu vyuo vyote kufunguliwa na wanafunzi wa kidato cha sita kurejea shuleni ili kujiandaa na mitihani ya kuhitimu elimu ya sekondari.  

“Maisha lazima yarudi kama ilivyokuwa zamani. Hata hivyo, naendelea kuwasihi Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari na pia kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalamu wetu wa afya kwasababu ni muhimu kuzingatia hilo,” amesema Rais Magufuli wakati akiagiza kufunguliwa kwa shughuli zote zilizokuwa zimezuiliwa ikiwemo ndoa. 


Zinazohusiana:


Aidha, amesema siyo tu Tanzania imefanikiwa kuushinda ugonjwa huo lakini pia kupunguza athari zake zikiwemo athari za kiuchumi.

“Kama mnavyofahamu Benki ya Dunia pamoja na Shirika la Fedha Duniani (IMF)yamebashiri kwamba asilimia 60 ya nchi za Afrika zilizopo kusini mwa jangwa la Sahara zitashuhudia ukuaji hasi yaani negative wa uchumi Mwaka 2020. 

Hata hivyo, sisi Tanzania kutokana na hatua tulizozichukua, uchumi wetu hautokua kwa negative. Utaendelea kukua vizuri angalau kwa asilimia 5.5 au zaidi,” amesema.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.