Serikali yatangaza ajira 3,633 za walimu masomo ya Biashara yakipewa kipaumbele

December 14, 2024 12:17 pm · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link
  • Wengine ni wa masomo ya Ushonaji, Uashi, Umeme, Ufundi magari, Uchomeleaji na Utengenezaji Vyuma, Sanaa.
  • Huenda uamuzi huo ukachochea ufaulu wa masomo ya Biashara.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imetangaza ajira 3,633 za walimu wa masomo mbalimbali ikiwemo ya Biashara, Ushonaji, Uashi, Umeme, Ufundi magari, Uchomeleaji na Utengenezaji Vyuma, Sanaa, Useremala, pamoja na Afya ya Wanyama.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Desemba 13, 2024 kwa niaba ya Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa imekaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 3,633.

Hata hivyo, Kwa mujibu wa taarifa hiyo yenye Kumb.Na.JA.9/259/01/B/109 zaidi ya asilimia 94 ya nafasi zilizotangazwa ni za walimu wa masomo ya Biashara wakiwa na nafasi 3,425.

Aidha, vigezo na sifa za muombaji vimeainishwa katika kila nafasi ambapo si lazima muombaje awe amehitimu chuo ngazi ya stashahada au shahada katika kada ya ualimu pekee hususan katika masomo ya ufundi kama Ushonaji, Uashi, Umeme, Ufundi magari, Uchomeleaji na Utengenezaji Vyuma.

Itakumbukwa, Novemba 23, mwaka huu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Adolph Mkenda alidokeza kuwa Serikali ipo mbioni kutoa kibali cha ajira 4,000 za walimu wa masomo ya biashara.

Chambuzi za matokeo ya kidato cha nne na cha pili ziliofanywa na Nukta Habari zilibaini kuna upungufu mkubwa wa vitabu pamoja na walimu wa masomo ya biashara jambo ambalo huenda imekuwa sababu ya wanafunzi kutofanya vizuri kwenye masomo hayo.

Huenda uamuzi huo wa Serikali kutoa ajira nyingi kwa walimu wa masomo ya biashara ukachochea kwa kiasi ufaulu wa masomo hayo muhimu katika kutengeneza wataalamu wa uchumi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
14 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
14 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV