Serikali ya Uganda haijatangaza fidia kwa majeruhi wa ajali iliyosababishwa na msafara wa Rais

September 16, 2022 6:51 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Hakuna taarifa rasmi kutoka ikulu ya Uganda inayoonyesha kuwalipa fidia majeruhi wa ajali.
  • Serikali ya nchi hiyo kupitia ukurasa wa Twitter imewataka  wananchi kupuuzia taarifa hiyo.

Dar es Salaam. Kama wewe ni mtumiaji wa mtandao wa Twitter hapana shaka umekutana na ujumbe unaosambaa kwenye mtandao huo  unaodaiwa kutoka Ikulu ya Uganda ukiahidi kutoa fidia kwa majeruhi wa ajali iliyosababishwa na msafara wa Rais Yoweri Museveni  Septemba 12, 2022. Ujumbe huo sio wa kweli.

Ujumbe huo uliosambazwa kupitia akaunti ya Twitter inayofanana na ile ya Ikulu ya Uganda umebeba maneno ya Kiingereza yanayosomeka:

 “Tutatoa fidia kwa waathirika wa ajali waliofariki lakini tunawaonya watumiaji wa barabara kujifunza kuheshimu msafara wa Rais, tutawagonga na kuwaacha barabarani ikiwa mnafikiri mna umuhimu kuliko maisha ya Rais.”

Kupitia ukurasa rasmi wa Twitter wa Ikulu ya Uganda taarifa hiyo imewekewa alama nyekundu ikimaanisha ni habari ya uzushi na wamewataka wananchi kupuuzia  ujumbe huo.

Tuliyobaini zaidi

Uchunguzi uliofanywa na timu ya NuktaFakti (www.nukta.co.tz) umebaini kuwa ukurasa rasmi wa Twitter wa Ikulu ya Uganda hauwajahi kuchapisha taarifa zozote kuhusu ajali au tamko lolote la kuwalipa fidia majeruhi wa ajali hiyo.

Neno “Tweet” kwenye kila ujumbe wa mtandao huu hukaa juu ya jina la akaunti (kama inavyoonekana hapo chini) na sio katikati kama inavyoonekana kwenye ujumbe huo wa uzushi unaosambaa.

Aina ya maandishi (font) iliyotumika kwenye ujumbe wa uzushi haifanani na aina za kawaida zinazotumika kwenye mtandao wa Twitter.

Pia matumizi ya lugha isiyo rasmi yaliyotumika kwenye ujumbe huo wa uzushi yanaashiria mwandishi siyo mtu aliyebobea kwenye mawasiliano ya taasisi kubwa kama Ikulu hivyo ujumbe huo wa uzushi si wa kweli.

Uamuzi wetu

Kupitia ushahidi ulioonekana hapo juu, ujumbe huu wa uzushi si wa kweli kuna uwezekano ukawa umetengenezwa kwa kutumia program hariri zenye uwezo wa kufuta na kuchapisha ujumbe mpya kwa kuiga ujumbe halisi akaunti husika.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.