Serikali kushusha tozo maendeleo ya ufundi (SDL)

June 11, 2020 2:23 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Zimeshushwa kutoka asilimia 4.5 hadi asilimia 4 ili kuwapunguzia waajiri mzigo na gharama za uendeshaji.
  • Kwa muda mrefu waajiri wamekuwa wakilalamikia uwepo wa kiwango kikubwa cha tozo hizo ambazo huathiri pia mapato yao.

Dar es Salaam. Serikali imependekeza kushusha kiwango cha tozo kwa ajili ya maendeleo ya ufundi stadi (Skills Development Levy) kutoka asilimia 4.5 hadi asilimia 4 ili kuwapunguzia waajiri mzigo na gharama za uendeshaji.

Waziri wa Fedha na Mipango Dk Philip Mpango amesema hatua hiyo inatarajiwa kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Sh42.07 bilioni.

“Lengo la marekebisho haya ni kuwapunguzia waajiri mzigo na gharama za uendeshaji wa shughuli zao na kutimiza azma ya kupunguza tozo hizi hatua kwa hatua bila kuathiri mapato kwa kiasi kikubwa,” amesema Dk Mpango.

Kwa muda mrefu waajiri wamekuwa wakilalamikia uwepo wa kiwango kikubwa cha tozo hizo ambazo huathiri pia mapato yao.

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Nukta TV

Mama Salama alivyombana Wanu kuhusu maslahi ya walimu wanaojitolea

Mama Salama alivyombana Wanu kuhusu maslahi ya walimu wanaojitolea

Nukta TV

Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Nukta TV