Safari ya mwisho ya Google Plus

February 4, 2019 9:50 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link

Muonekano wa ukurasa wa Google+ ikiwa ni zimebaki siku chache kabla ya kufutwa kabisa April 2 mwaka huu. Picha|Daniel Mwingira.


  • Google+ imekosa ushawishi kwa watumiaji wake ambapo asilimia 90 ya wafuasi wake  walikuwa wanatumia sekunde tano kuingia na kutoka katika mtandao huo.
  • Google imesema kufikia Aprili mbili mwaka huu,  kurasa zote za Google+ zitaondolewa sambamba na maudhui yote zikiwemo picha, video na kumbukumbu zote za watu binafsi. 

Dar es Salaam. Kampuni ya Google imetangaza kuanzia leo (Februari 4, 2019) haitaruhusu mtu yeyote kufungua akaunti mpya katika mtandao wa Google+, ikiwa ni hatua za kukamilisha mchakato wa kuufuta kabisa mtandao huo ifikapo Aprili mwaka huu. 

Uamuzi kuifuta kabisa Google+ ulitangazwa mwishoni mwa mwaka 2018 huku sababu kubwa zilizotolewa na kampuni hiyo ya teknolojia duniani zinaeleza kuwa Google+ imekosa ushawishi kwa watumiaji wake ambapo asilimia 90 ya wafuasi wake  walikuwa wanatumia sekunde tano kuingia na kutoka katika mtandao huo. 

Kufutwa kwa mtandao wa Google+ ulioanzishwa mwaka 2011 kunafuata nyayo za huduma ya ‘Google Fusion’ ambayo nayo iko mbioni kuondolewa mwaka huu.    

Google imesema kufikia Aprili mbili mwaka huu,  kurasa zote za Google+ zitaondolewa sambamba na maudhui yote zikiwemo picha, video na kumbukumbu zote za watu binafsi. 

Hata hivyo watumiaji wa mtandao bado wana nafasi ya kuondoa taarifa na kumbukumbu muhimu katika mtandao huo kwa kufuata maelekezo yanayopatikana katika dawati la usaidizi la “Google+ Help Page’ kabla tarehe ya mwisho haijafika.

Kwa mujibu wa Google, maudhui mengine ya Google+ yataweza kupatikana kwa watumiaji wa mtandao wa kutunza nyaraka za G Suite.


Zinazohusiana: 


Duru za usalama mtandaoni zinaeleza kuwa sababu nyingine ya Google+ kufutwa ni kushindwa kudhibiti taarifa wa watumiaji zaidi ya 500,000 wa mtandao huo zilizodukuliwa na kuhatarisha usalama wao mtandaoni.  

Mdau wa  mitandao ya kijamii, Kenney Mmari amesema kuondoka kwa Google+ kunaweza kuwa na matokeo hasi kwa watumiaji waliopo katika maeneo mbalimbali duniani.  

Amesema Google+ ni mtandao wa kipekee uliowakutanisha watu wenye maono yanayofanana na kujenga mtandao wa mawasiliano ya kibiashara, kazi na taaluma, ambapo kufutwa kwake kutaondoa fursa hiyo ya kuwasiliana kwa urahisi.

“Unajua mtandao wa kijamii wa Google + ulikuwa kama Linkedlin sasa kufutwa kwake kutaondoa fursa kwa tabaka hilo la watu ambao tayari lilishajiwekea mtandao wao huko,” amesema Mmari

Pia amebainisha kuwa kundi lingine litakaloathirika ni lile la wachapishaji wa maudhui mtandaoni (Bloggers) ambao hawatapata nafasi ya kutumia Google+  kuandika na kusambaza maudhui kwa watu wengi.

Hata hivyo, kufutwa kwa mtandao huo ni fursa kwa kampuni zingine za teknolojia kubuni mtandao utakaowakutanisha watu pamoja kama WhatsApp na Facebook.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV