Rwanda yazifuata Kenya, Tanzania kutoa pasipoti za kielektroniki

June 29, 2019 9:50 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Inakua nchi ya nne katika jumuiya ya Afrika Mashariki kutoa pasipoti hizo kwa raia wake.
  • Pasipoti hiyo itarahisisha safari na biashara ya mipakani katika jumuiya hiyo.

Hatimaye Rwanda imeanza kutoa pasipoti ya kielektroniki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa raia wake ikiwa ni hatua ya kurahisisha na kuongeza wigo wa safari na biashara ya mipakani miongoni mwa nchi wanachama wa jumuiya hiyo. 

Rwanda inakuwa nchi ya nne katika jumuiya hiyo kutoa pasipoti za kielektroniki  ikiungana na nchi za Kenya, Tanzania na Uganda ambazo tayari zinatoa pasipoti hizo kwa raia wake.  

Uzinduzi wa pasipoti za kielektroniki katika nchi ya Rwanda umefanyika jana (Juni 29, 2019) jijini Kigali na Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji wa nchi hiyo, Francois Regis Gatarayiha. 

Akizungumza na vyombo habari, amesema pasipoti hiyo ya Afrika Mashariki itachagiza biashara na usafiri wa mipakani na kuimarisha ushirikiano wa jumuiya hiyo. 

Pasipoti hiyo imeunganishwa na ‘chip’ ndogo ya kielektroniki ambayo ina taarifa muhimu za mmiliki ikiwemo jina, mwaka wa kuzaliwa na taarifa nyingine za makazi. 

Gatarayiha amesema pasipoti hiyo imezingatia maelekezo ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) na kuifanya pasipoti hiyo kukubalika duniani. 


Soma zaidi: 


Uamuzi wa kutumia pasipoti za kielektroniki zinazofanana ulifikiwa katika kikao cha 17 cha wakuu wa nchi wa jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika Machi 2016 jijini Arusha. 

Pasipoti za kielektroniki zinatajwa kuwa ni salama zaidi kuzitumia kwa sababu zimeunganishwa na mifumo ya usalama mtandaoni, jambo linalofanya iwe vigumu kwa mtu kuiba au kughushi taarifa za mtumiaji zilizopo katika kanzi data (data base).

Lakini ni fursa kwa wananchi wa Afrika Mashariki hasa katika biashara inayofanyika mipakani na inarahisisha utambuzi wa raia kwa haraka katika vituo vya uhamiaji vilivyopo kwenye viwanja vya ndege na mipakani.

Hata hivyo, pasipoti hizo mpya ambazo zinachukua nafasi ya zile za zamani zinawahakikishia wananchi wa Afrika Mashariki kuishi na kufanya kazi katika nchi wanachama bila vikwazo. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV