Ruvuma inavyokimbiza uzalishaji wa mahindi Tanzania
- Inaongoza kwa uzalishaji wa zao hilo.
- Mwaka 2019/20 ilizalisha tani 498,685.
Dar es Salaam. Kwa mujibu wa ripoti ya Sensa ya Taifa ya Kilimo ya mwaka 2019/20 ni Ruvuma ni mkoa unaongoza kwa uzalishaji wa mahindi Tanzania Bara.
​Ripoti hiyo inaeleza kuwa mwaka 2019/20, mkoa huo ulizalisha tani 498,685 sawa na asilimia 7.7 ya mahindi yote yaliyozalishwa mwaka huo ambayo yalikuwa tani milioni 6.5.
Mikoa mingine iliyokuwa na uzalishaji mkubwa ni Manyara ikishika nafasi ya pili ikifuatiwa na Tanga na Tabora.
