Corona: Zingatia haya unapopokea mgeni nyumbani

March 10, 2021 12:41 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kuendeleza tabia za kujikinga na corona hata mnapokuwa nyumbani ikiwemo kuvaa barakoa na kunawa mikono.

Dar es Salaam. Miaka mitatu iliyopita, kupokea mgeni nyumbani huenda lilikua jambo la kheri na wageni walipokelewa kwa makumbato mazito kutoka kwa wenyeji wakifurahia ujio wao huku watoto wakishangilia kwa mapokezi tofauti tofauti na kupokea mizigo ya mgeni.

Hata hivyo, huenda tamaduni hizo zikabadilika katika kipindi hiki cha mpito cha ugonjwa wa Corona ambapo kila mtu anatakiwa kuchukua tahadhari kwa kuepuka na mgusano kati ya mtu na mtu ama kitu na mtu bila kuwepo ulazima.

Hata hivyo, maisha ni lazima yaendelee ikiwa ni pamoja na kupokea wageni hasa pale panapokuwa na ulazima wa ugeni huo. Zipo tahadhari ambazo unaweza kuzichukua unapopokea mgeni. Siyo unyanyapaa, ni tahadhari.

Tazama video hii kujifunza zaidi:

                        

Enable Notifications OK No thanks