Rais Samia amteua Mcheche Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania

June 13, 2025 10:10 am · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Rais  wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani George Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania kuchukua nafasi ya Prof Ibrahim Hamis Juma ambaye amestaafu baada ya kuhudumia mhimili huo wa dola kwa miaka minane. 

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu leo Juni 13, imebainisha kuwa  uapisho wa Masaju utafanyika Juni 15, 2025 Ikulu, Chamwino Dodoma.

Kabla ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo Jaji Masaju amewahi kuwa mshauri wa Rais Jakaya Kikwete katika masuala ya kisheria na baadae alihudumu kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali.


Januari 22, mwaka huu Jaji Masaju aliapishwa na Rais Samia kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Enable Notifications OK No thanks