Rais Magufuli ataka Serikali kutojiingiza sana uwekezaji sekta binafsi

June 25, 2019 3:00 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Rais Magufuli aliyekuwa akizungumza leo (Juni 25, 2019) wakati akizindua ghala na mitambo ya kuchakata gesi ya majumbani (LPG) iliyoko wilayani ya Kigamboni, Jijini Dar es Salaam. Picha|Mtandao.


  • Amewataka wajikite kukusanya mapato na kuweka utaratibu mzuri wa wawekezaji kufanya shughuli zao.
  • Wametakiwa kuzungumza na wawekezaji kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili.
  • Serikali imesema itaendelea kuweka mazingira mazuri ya biashara ili kuvutia wawekezaji.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amewataka watendaji wa Serikali kutojiingiza na kudhibiti  uwekezaji katika sekta binafsi bali wajikite katika kukusanya mapato na kuweka utaratibu mzuri utakaozifaidisha pande zote mbili. 

Rais Magufuli aliyekuwa akizungumza leo (Juni 25, 2019) wakati akizindua ghala na mitambo ya kuchakata gesi ya majumbani (LPG) iliyoko wilayani ya Kigamboni, Jijini Dar es Salaam, amesema wakati mwingine upande wa Serikali umekuwa unakimbilia kudhibiti sekta binafsi lakini baadaye unaharibu maana nzima ya uwekezaji.

“Wizara (Wizara ya Nishati) na wawekezaji ni vyema mkakaa na mkakubaliana katika taratibu nzuri za  ‘win win situation’ (maslahi ya pande zote) kwa sababu saa nyingine upande wa Serikali tunakimbilia sana kukusanya na kujifanya tunaweza kudhibiti halafu baadaye tunaharibu,” amesema. 

Agizo hilo la Rais linakuja baada ya Wizara ya Nishati kuandaa mpango wa pamoja wa uagizaji wa gesi ya mitungi (LPG) ili kudhibiti usambazaji na bei elekezi ya gesi hiyo inayotumika zaidi katika shughuli za nyumbani. 

Hata hivyo, Rais amesema hakuwa na taarifa na mpango huo mpya lakini Serikali na wawekezaji wakae pamoja kuangalia namna ya kupata haki kwa usawa kupitia uagizaji huo.

“Ninachotaka kusema ni kwamba ninyi wote mzungumze ili kusudi Serikali ipate haki yake iliyo ya haki, lakini Serikali nayo isijiingize sana kwenye uwekezaji wa sekta binafsi kwa sababu walishindwa Serikali kuleta hii gesi.

“Mnakimbia haraka haraka kufanya nini, badala ya kukaa na kukusanya revenue (mapato), kwa hiyo mambo haya yote tuyaangalie kwa pamoja,” amesema Rais Magufuli.


Soma zaidi:


Hata hivyo, amesema wataendelea kuweka mazingira wezeshi ikiwemo kuboresha miundombinu ya barabara na uzalishaji wa nishati ya umeme wa kutosha ili kuvutia wawekezaji kufanya biashara zao kwa uhuru. 

“Bei ya umeme kwa Watanzania na wawekezaji tutaishusha ili wawekezaji wengi waweze kupata faida katika miradi yao watakayokuja kuwekeza katika nchi hii,” amesema Rais.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV